Sunday, July 24, 2011


Sherzinger: Hamilton hajanichumbia

Mwanamuziki Nicole Scherzinger amekanusha vikali kuwa amechumbiwa na dereva wa magari ya Formula One, Lewis Hamilton.
Sherzinger aliandika katika mtandao wa mawasiliano wa Twitter kukanusha vikali taarifa hizo zilizosambaa kwa kasi.
Nicole aliandika; "Lewis na mimi tuliamka asubuhi na kusoma taarifa kuwa tulikuwa tumevalishana pete."
Baba wa Nicole, Alfonso Valiente ndio mtu aliyechangia kuenea kwa uvumi huo.
ìWatu hawa wamechumbiana na ninampenda sana mkwe wangu Lewis Hamilton."

Charlize, Reynolds wabambwa

Paparazzi hivi karibuni waliwanasa nyota wa filamu, Charlize Theron na Ryan Reynolds wakiwasili muda mmoja katika Uwanja wa Ndege wa Los Angeles, Marekani.
Kitendo hicho kilizidi kuthibitisha kuwa Charlize na Ryan wana uhusiano wa mapenzi.
Watu hao wawili wamekuwa wakificha suala la wao kuwa na uhusiano wa mapenzi.
Charlize ameapa kutokwenda mahali popote akiwa amefuatana na Ryan.
Mkali huyo wa filamu alieleza huwa hana utaratibu kufuatana na mtu wake kila mahali anapokwenda.
Naomi awapiga jeki Red Cross

Mwanamitindo Naomi Campbell ametoa kitita cha pauni 94,000 (sh. 231 milioni) kwa ajili ya Shirika la Msalaba Mwekundu.
Campbell ametoa fedha hizo ili kusaidia watu walioathirika na kimbunga cha tsunami nchini Japan.
Naomi hivi karibuni aliandaa maonyesho ya mavazi huko Cannes, Ufaransa kwa ajili ya kuchangia fedha za kusaidia watu wa huko Japan.
"Mara nyingi tumekuwa tukiandaa maonyesho ya mavazi sehemu mbalimbali duniani ili kusaidia watu wenye matatizo mbalimbali."
Mastaa wa fani mbalimbali walichangia fedha ili kusaidia watu wa Japan, ambao pia waliathirika na kulipuka kwa mitambo ya nguvu za nyuklia.

Kim Kardashian kufunga ndoa Agosti

Harusi ya mwanamitindo Kim Kardashian na nyota wa mpira wa kikapu, Kim Humphries itakuwa Agosti 20, mwaka huu.
Kardashian alisema; ìKwa kweli nimekuwa nikiota kuolewa tangu nikiwa msichana mdogo.î
Katika sehemu ya maandalizi ya harusi hiyo, Kim alifanya vikao vingi na mahojiano na televisheni jijini New York.
Sasa ametua jijini Los Angeles ili kuendelea na maandalizi ya shughuli hiyo.
Atuhumiwa kuvunja ndoa ya Lopez

J. Lo na Levy, pia alishiriki katika tamthiria ya ITV
'Don't Mess with my Angel' au Marichuy

Mwanamitindo William Levy ndio anatuhumiwa kuvunja ndoa ya Jennifer Lopez.
Mwanamuziki Lopez, ambaye ni maarufu kwa jina la J.Lo alitangaza kutengana na mumewe Marc Anthony wiki iliyopita.

Enzi za ndoa yake na Mack Anthony

Kuna taarifa kuwa J.Lo alikuwa na uhusiano wa mapenzi wa siri na Levy.
Mwanamitindo huyo alishiriki katika video ya wimbo wa J.Lo wa ìIím Into Youî.
Levy, ambaye aliachana na mkewe mwezi mmoja baada ya kurekodi video, amekanusha vikali taarifa hizo. hiyo


"Ninachoweza kusema Jennifer si mpenzi wangu bali uhusiano wetu ni wa kikazi zaidi."


Abramovich akodisha boti lake

Mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich (pichani juu), anakodisha boti yake kwa bei ya kutisha ya pauni 1.25 milioni (sh. 178 milioni za Kenya)kwa wiki.
Abramovich alinunua boti kwa kiasi cha pauni milioni 750 milioni (sh. 107 bilioni za Kenya) ili kulipia boti hiyo inayoitwa Eclipse.
Boti hiyo ni ya aina yake kwani ina vifaa ya kurusha makombora ya kivita chini yake.
Gharama ya kukodisha kwa siku ni kiasi cha pauni 175,000 (sh. 25 milioni za Kenya). Gharama hizo zinajumuisha posho za wafanyakazi 70, kutumia helikopta mbili, bwawa la kuogelea, gym na saluni.
Boti hiyo ina vyumba 15 vinavyoweza kuingiza wageni 30, mabafu ya kisasa na televisheni za kisasa.

Gharama ya kuhudumia boti hiyo ni kiasi cha pauni 50 milioni (sh. 7.1 bilioni za Kenya) kwa mwaka. Gharama ya mafuta ni pauni 400,000 (sh. 57 milioni za Kenya)



Demu mwingine amwanika Cole

Mwanamke mwingine ameibuka kufichua kuwa alilala na Ashley Cole wakati akijaribu kumrudia mkewe wa zamani, Cheryl.
Collette McBarron, ambaye ni mwanamitindo alisema alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na beki huyo wa Chelsea na England.
Kitendo hicho kitazidi kumchafua Cheryl, ambaye katika siku za karibuni amekuwa akisaka suluhu na mumewe Cole.

Huyu ndiye mtuhumiwa mwenyewe, Ashley Cole
Collette, ambaye aliwahi kuwania taji la Mrembo wa Ireland: "Kwa kweli ninaposikia habari ya Cole kujirekebisha nabaki nashangaa."
Mrembo huyo, ambaye alikuwa jeshini, alisema ana picha za kuthibitisha uhusiano wao na Cole.
Mhudumu wa kwenye ndege, Kerry Meades alikaririwa na gazeti la Sunday Mirror la Uingereza wikiendi iliyopita akidai pia alikuwa anatembea na Ashley wakati akisaka suluhu na mkewe Cheryl, ambaye waliachana.


Fally Ipupa avuruga mambo Mombasa


MWANAMUZIKI maarufu kutoka Congo, Fally Ipupa alisababisha vurugu katika ukumbi wa Mamba Disco aliposusia kuhudhuria tamasha hilo lililongojewa na wakazi wengi wa mjini Mombasa kwa hamu na ghamu.
Inadaiwa kuwa Fally Ipupa alisusuia shoo hiyo kwa kuwa hakupewa malipo yake kwa wakati unaofaa.
Ni mara ya pili kwa msanii huyu kususia shoo mjini Mombasa, zote zikiwa zimeandaliwa na promota Jules Nsana wa Nsana Promotions.
Muda mfupi kabla ya saa tisa za alfajiri, Fally Ipupa aliandika kwenye Facebook kuwa: "For Organisational reasons, the organisers cancel the show in Mombasa."
Mashabiki walianza kumshambulia DJ Collo na kuharibu vifaa vyake kwa hasira, huku wengine wakiyarushia mawe magari yaliyokuwa yameegeshwa nje ya ukumbi huo.
Wafanyakazi katika ukumbi wa Mamba walilazimika kubadilisha mavazi yao ya kazi ili wasiweze kutambulika kiurahisi na mashabiki wa Ipupa, mpaka wakati ambao polisi waliingilia kati na kuidhibiti hali hiyo ya kutatanisha.
Bendi ya msanii huyo ililazimika kwenda jukwaani ili kuwatuliza mashabiki ambao kwa wakati huo walikuwa wanadai kurudishiwa pesa zao, wakitishia kumfungulia mashtaka Fally Ipupa pamoja na mmiliki wa klabu hiyo.


Siku moja kabla ya tukio hilo, msanii huyo alikuwa katika ukumbi mmoja jijini Nairobi katika tamasha ya Rhumba Night ambako pia alizua hali ya mshike mshike na isitoshe anadaiwa kuwapokonya baadhi ya wanahabari kanda zao.
Waandalizi wa tamasha hiyo walisita kutoa maoni yao kuhusu yaliyojiri usiku huo katika ukumbi wa Mamba mjini Mombasa.

Wednesday, July 20, 2011

Hii ni sehemu mojawapo muhimu ya jiji la Dar! Hebu angalia....

Mtaro ukiwa umefurika maji taka katika barabara ya Shaurimoyo eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam,ambapo ni hatari kwa magonjwa ya mlipuko pia wafanyabiashara wa eneo hilo wameendelea na shughuli zao bila kujali athali za kiafya zinazoweza kutokea.Picha na Michael Jamson




Monday, July 18, 2011

Hawa ndio wadau wangu




Hapa ni Aliamini Adam aka Mzee wa Mombasa, Shilwa Mboma aka Bakhresa na Mkolo Kimenya- huyu ndiye aliyepiga picha kasoro hii tu!


Hawa niliyokuwa nao ni wadau na wafanyakazi wenzagu, hawa ndiyo wanasababisha unasoma gazeti linaloongoza na kuaminiwa Tanzania- Mwananchi na lilie gazeti bora la Michezo Afrika Mashariki- Mwanaspoti. Kushoto ni Elizabeth Mushi aka Asha Ngedere na Shilwa Mboma aka Bakhresa.


Hapa ndio desk zima, wote hawa kwa umoja ndio timu ya madesigner wa Mwananchi na Mwanaspoti


I mean woooteee!

Friday, July 15, 2011


Lady Gaga apigwa mawe

SI siri mwanamuziki Lady Gaga ana mashabiki kibao lakini ana maadui wengi pia.
Gaga alikutana na watu wanaomchukia pale alipotua Australia na kujikuta akipigwa na mayai.
Alikutwa na mkasa huo wakati akiwasili katika klabu ya usiku ya ARQ huko Sydney, Australia.
Gaga alikuwa amezingirwa na mashabiki wake na walinzi lakini shabiki anayemchukua alirusha yai ambalo lilimpiga kichwani.
Mtu huyo anadaiwa kuchukizwa na kitendo cha Gaga kupewa uraia wa Australia na Meya wa Sydeny.

Foxy Brown kushtakiwa

FOXY Brown atapandishwa kizimbani baada ya kuvunja amri ya mahakama. Ameingia matatani baada ya kumtukana jirani yake kinyume na amri ya mahakama. Waendesha mashtaka wanadai kuwa Brown alivunja amri ya mahakama Julai 2010 baada ya kumsemea ovyo jirani yake.
Kibaya zaidi wakati akimtukana jirani huyo, Arlene Raymond, Brown aliinama na kuonyesha makalio yake na nguo ya ndani huku akiendelea kumtukana.
Watu hao wawili wamekuwa na bifu la muda mrefu. Kuna amri ya mahakama inayomzuia Brown kuzungumza na jirani huyo.

Lil Kim ajipanga upya

RAPA Lilí Kim anafanya kazi ya ziada ili kuibua kitu kipya.
Kim anataka kuhakikisha kuwa anarejea kwa kishindo katika gemu la hip hop.
Hivi karibuni alisherehekea kutimiza miaka 37, akiahidi kutoa singo mpya na albamu ya tano.
Kim amepanga kuachia wimbo wa "Looks Like Mone", ambao umetengenezwa na Rockwilder.
Mashabiki wake wanataka kuona Kim anaweka matatizo yake pembeni na kutoa nyimbo kali.

Nicki Minaj apigwa konde

RAPA Nicki Minaj alipigwa ngumi na mchumba wake Safaree baada ya kutokea ubishi katika hoteli moja huko Dallas.
Minaj alipigwa ngumi hiyo mdomoni na Safaree wakati wakiwa chumbani mwao.
Minaj, hata hivyo, amedai kuwa hana mpango wa kufungua mashtaka dhidi ya mtu huyo.
Mara ya kwanza rapa huyo hakutaka kusema alikuwa anagombana na nani ingawa ilikuja kujulikana alikuwa Safaree.
Inadaiwa ubishi wa watu hao wawili ulitokea katika bwawa la kuogelea la hoteli hiyo.
Mzozo ulizidi wakaenda kwenye chumba chao na ndipo Safaree akarusha ngumi.
Minaj aliomba wafanyakazi wa hoteli kuita polisi baada ya kutokea ugomvi huo na walifika mara moja na Safaree alikamatwa ingawa hakufunguliwa mashtaka.


Shakira, Pique wafunga baa

Mwanamuziki Shakira na mpenzi wake Gerard Pique walifunga baa baada ya kujirusha kisawasawa huko Miami, Marekani.
Shakira na Pique anayechezea Barcelona ndio walikuwa watu wa mwisho kuondoka katika klabu ya usiku ya Miami Beach.
Walikuwa na rafiki zao, ambao walifunga nao safari ya mapumziko nchini Marekani.
Watu hao wawili walionekana wamechoka wakati walipokuwa wanatoka nyakati za alfajiri kwenye ukumbi huo wa disko usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.
Walikuwa muda mwingi wakicheza disko na watu wengi walianza kuondoka mapema lakini wao walikaa hadi mwisho.
Shakira na Pique walitoka baadaye wakisindikizwa na walinzi na wapambe kibao.

NI uchakachuaji kwa kwenda mbele!


Gari la Mkuu wilaya ya Serengeti Mkoani Mara likifanyiwa matengenezo baada ya kuwekewa mafuta yaliyochakachuliwa kwa maji mjini Mugumu juzi. Jumla ya magari sita ya watu binafsi na serikali yalishindwa kutembea kutokana na kuwekewa mafuta hayo katika gereji moja (juna tuanalo).


Ukaguzi: Nani mwenye kitambi??


Ofisa wa Jeshi nchini Japan akikagua kikosi maalumu cha ulinzi kabla ya sherehe ya kumkaribisha Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Marekani, Mike Mullen iliyofanyika katika uwanja wa Wizara ya Ulinzi nchini humo jana. Mullen anapewa heshima hiyo kutokana na mchango wa kijeshi aliyoutoa kwenye Jeshi la Japan.

Tuesday, July 12, 2011


Kweli Tanzania kubwa!!


Abiria waliokuwa wakisafiri kati ya Arusha, Manyara na Singida, wakitazama greda la ilikikokota roli lililoshindwa kupanda mlima Mabangi uliopo kijiji cha Masakta Wilaya ya Hanang’, kutokana na uzito uliokithiri na kusasabisa abiria hao na magari mengine kukwama kwa zaidi ya saa mbili, kabla ya mkadarasi anayejenga barabara hiyo kulivuta kwa kutumia greda.

Kweli hawa tunaowachagua wanauchungu na sisi??!!

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu akifatilia wakati wabunge wakichangia mjadala wa kupitisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2011/2012, mjini Dodoma juzi.

Kaimu Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni, Samuel Sitta (katikati), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Mwita (kushoto) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wasira wakiwandani ya ukumbi wa bunge huku viti vingi vya mawaziri vikiwa wazi wakati wabunge wakichangia mjadala wa kupitisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2011/2012, mjini Dodoma jana.


Viti vitupu hata upinzani!


Wabunge wakiwa ndani ya ukumbi wa bunge wakati wa kuchangia mjadala wa kupitisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2011/2012, mjini Dodoma jana.

Abbas: Mguu wagu unanitesa


Abbas Abdalaah (31) aliapoanza kuvimba uvimbe mdogo katika mguu wake wa kulia hakujua kuwa ulikuwa ni mwanzo wa ugonjwa ambao hatimaye ungemfanya ashindwe kutembea.

Ugonjwa huo ambao mpaka sasa haujulikani, umemfanya Abbas kulala kitandni muda wote akilazimika kubebwa na watu watano kumpeleka nje kujisaidia.


Matumaini aliyokuwa nayo ya kupata tiba ya ugonjwa wake, yameanza kutoweka baada ya msamaria aliyejitokeza kumpeleka Hospitali ya Seliani mjini Arusha kushindwa kutimiza ahadi yake.



Abbas ambaye ni Mkazi wa Kijiji cha Kiru Ndogo, anasema vurugu za wananchi na wawekezaji wa Bonde la Kiru, Wilaya ya Babati mkoani Manyara, ndizo anaona zimesababisha mpaka sasa asipate msaada.

“Vurugu hizi zilizoaanza Machi mwaka huu , ndizo zilizosabisha leo niwe bado hapa sina msaada, kwani mmoja wa wawekezaji katika Bonde hili alikuwa ameaahidi kunisaidia kunipeleka hospitali ya Seliani," anasema kwa uchungu akiwa amelala katika kitanda chake kilichopo sebuleni kwenye nyumba ndogo ya nyasi ya Bibi yake, Zuhura Abdalah.

Akisimulia historia ya ugonjwa wake huo, anasema alianza kuvimba kiumbe kidogo katika mguu wake mwaka 2005, wakati huo akiwa mchezaji mzuri wa mpira wa miguu kijiji hapo.

Anasema hakuwa na wasiwasi kwamba huo ungekuwa ugonjwa mkubwa ambao ungemfikisha hapo alipo.


Taratibu mguu ulianza kuvimba, hali ambayo ilimfanya baba yake mzazi, mzee Abdallah Juma mwaka 2008, kumpeleka Hospitali ya Hydom, Wilaya ya Mbulu ambako baada ya kumchunguza hawakuona ugonjwa, ingawa mguu ulikuwa umevimba.

“Hydom hawakuona ugonjwa, nikawauliza mbona bado mguu umevimba kwa nini hamuoni tatizo, wakanishauri nirudi nyumbani, “ anasimulia kwa uchungu kijana huyu mchangamfu.

Ingawa madaktari katika hospitali hiyo hawakuona tatizo lolote katika mguu wa Abbas, lakini mguu mzima ulizidi kuongezeka unene, mwaka 2009 wazazi wake wakaamua kumpeleka Hospitali ya Mission ya Dareda, Wilaya ya Babati mkoani Manyara.

Huko waligundua alikuwa na matatizo katika seli za mwili hivyo wao hawakuwa na uwezo wa kumtibu na kumshauri aende Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyopo Moshi mjini mkoani Kilimanjaro.

Anasema mwaka uliofuatia alikwenda KCMC ambako alifanyiwa uchunguzi na matokeo yalionyesha kwamba alikuwa na matatizo ya maji kujaa katika mguu na pia alikuwa na tatizo la nyama kuongezeka katika mguu wake.

Abbas anasema baada ya kungulika tatizo hilo aliuzwa na daktari wake kama ana uwezo wa kulipia matibabu ya ugonjwa wake nje ya nchi, lakini alisema hana uwezo.

“Baada ya kueleza kuwa sina uwezo, basi huo ukawa ndio mwisho wa uwezo wao kunisaidia, nilirejea nyumbani nikiwa bado nina uwezo wa kutembea mwenyewe,” anasema.

Hata hivyo akiwa amekata tamaa ya kupata matibabu aliendelea kuishi huku akifanya shughuli zake za kila siku kwani mbali ya mguu kuendelea kuvimba , lakini hukuwa akisikia maumivu.

Machi mwaka huu ndio mwezi ambao utabaki katika kumbukumbu zake zaidi kijana huyu, kwani ndipo aliposhindwa kutembea na kuwa mtu kulala kitandani.

Tangu wakati huu kasi ya mguu kuvimba iliongezeka huku akiwa hawezi hata kusimama kwani akitaka kutoka nje ya nyumba anatakiwa kubebwa na vijana watano wenye nguvu. Mbali ya kuvimba sasa ana kidonda ambacho kinamsumbua katika mguu huo.



Sasa walahu amefikishwa hospitali kwa ajili ya huduma


Abbas Abdalaah akiwa mapokezi hospital ya Rufaa ya KCMC iliyopo Moshi mjini mkoani Kilimanjaro akishushwa kweye gari kuingia wodini kupata matibabu.

Yangaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!

Hayawi hayawi sasa yamekuwa. Alikuwa ni mshambuliaji Keneth Asamoah aliyeingia akitokea benchi katika dakika 15 za mwisho wa mchezo aliunganisha vizuri kwa kichwa krosi makini ya Rashid Gumbo na kuipa Yanga ubingwa wa nne wa michuano ya Kagame Castle Cup baada ya kuichapa Simba bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

TFF tumewaona mashbiki hao, msitupige changa hapo!

Kaseja umeiona hii!

Shamrashamra tulizianza mapemaaaaa!
Utamu wa ushindi!
Teh... Teh... Teh... Teh....!
Angalia mpanga mzee akapagawa!

Monday, July 11, 2011

Mheshimiwa Sugu kizimbani Mbeya


Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chadema, Joseph Mbilinyi na wezanke wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mbeya kwa tuhuma za kuandaa mkutano wa hadhara kinyume cha sheria.

Mbilinyi ni mbunge wa saba wa Chadema kupanda kizimbani akitanguliwa na wabunge wenzake, Freeman Mbowe (Hai), Godbless Lema (Arusha), Joseph Selasini (Rombo), Philemon Ndesamburo (Moshi Mjini), Tundu Lissu (Singida Mashariki) na Esther Matiko (Viti Maalum), ambao wanashtakiwa kwa tuhuma tofauti katika mahakama mbalimbali nchini.

Mbilinyi maarufu kwa jina la ‘Mr II au Sugu’ alifikishwa mahakamani jana pamoja na wenzake ambao ni Mwenyekiti wa Chadema, Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako na Katibu Mwenezi wa chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini, Job Zebedayo Mwanyerere.

Mama Salma azindua uchangiaji madawati

Mke wa Rais Salma Kikwete, akizindua nembo ya Taasisi isiyokuwa ya Kiserikari ya Hassan Maajar Trust, itakayoanzisha kampeni ya kusanya fedha za kukununulia madawati kwa ajili ya shule za msingi na sekondari Kwanza kushoto ni Mjumbe wa Bodi Sharriff Maajar na Mwenyekiti wa Mfuko Balozi Mwanaidi Sinare Maajar.


Mke wa Rais Jakaya Kikwete, mama Salma Kikwete, amezindua kampeni ya kumaliza tatizo la madawati katika shule za umma nchini.

Kiasi cha Sh3 bilioni kinatarajiwa kukusanywa chini ya kampeni ya miaka miwili.

Kampeni hiyo inayoendeshwa na Taasisi ya Hassan Maajar Trust (HMT), ambayo Mwenyekiti wake ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mwanaidi Maajar, ilizinduliwa jana jijini Dar es Salaam.

"Lengo la kampeni hii ni kukusanya Sh3 bilioni katika kipindi cha miaka miwili au mitatu ijayo, fedha zitakazochangwa zitatumika kununulia madawati kwa ajili ya shule za umma za msingi na sekondari, ili kuboresha elimu nchini," alisema Balozi Maajar.


Waziri apokelewa kwa mabango ya malalamiko

Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, akimsililiza Diwani wa Kata ya Nairokanoka, wilayani Ngorongoro, Edward Maura (kulia), alipokuwa akitoa maelezo kuhusu hali ya njaa katika kata yake juzi. Kati kati ni Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Ngorongoro, Benard Murunya na wa pili kushoto ni, Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji wa Ngorongoro, Metui ole Shaudo.


Wananchi wa Kijiji cha Nainokanoka ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), juzi walimpokea kwa mabango yenye malalamiko mbalimbali, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.

Mabango hayo ni pamoja na yaliyokuwa na ujumbe wa kuishinikiza serikali, iwape ajira ya asilimia 75 katika mamlaka hiyo.

Mengine yalikuwa na ujumbe uliohoji usawa katika elimu, njaa inayowakabili, utegemezi na mbadala wa kuzuiwa kufanya shughuli za kilimo ndani ya hifadhi.

Akizungumza baada ya kuyasoma mabango hayo, Waziri Maige alitoa maelezo kuhusu malalamiko ya wananchi hao.

"Nimesoma mabango yote lakini sehemu kubwa ya malalamiko yenu, tunaweza kuyapatia ufumbuzi hasa kwa kuzingatia kuimarika kwa mahusiano,kati ya wananchi, Baraza la Wafugaji na NCAA,"alisema Maige.