Tuesday, September 27, 2011

Hatimaye mdogo wetu aenda India kwa matibabu

Mgonjwa anayesumbiliwa na matatizo ya moyo kwa zaidi ya miaka 11 , Sesilia Edward (katikati) akisindikizwa na Muuguzi wa Hospitali ya Regency, Mary Gomes (kushoto) na Dk Christopher Lucas, muda mfupi kabla ya kuondoka kwenda india kwa matibabu.

Lazima kieleweke!

Mkazi wa Manispaa ya Morogoro akiwa amebeba kiroba cha unga kichwani huku akiwa amepakiza kingine kwenye usukani wa baiskeli, eneo la Kituo cha daladala ziendazo nje ya manispaa hiyo.

Igunga bado, hebu tuombe mambo yaende vizuri Inshaallah

Waumini wa madhehebu ya dini ya Kikristo wakiwa kwenye maombi maalum ya kuombea Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga unatalajiwa Jumapili hii kufanyika kwa amani na utulivu, maombi hayo yalifanyika kwenye uwanja wa Sokoine mjini Igunga juzi jioni.

Ajali haina kinga, IGP chupu chupu

Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Said Mwema (kulia) akifalijiwa na msamaria mwema baada ya kunusurika katika ajali ya gari iliyotokea juzi katika Barabara ya Kivukoni Front, mbele ya Ofisi za Takwimu na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Gari ya IGP iliyokuwa ikitokea Magogoni iligongana na gari ndogo.

Malori saba ya sukari yakamatwa Tarime

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tarime/Rorya, Deusdedit Kato (kushoto), akiwa na maofisa wa jeshi hilo mbele ya magari yaliyokamatwa kwa madai ya kukutwa yamebeba sukari kupeleka kuuzwa nchini Kenya.

Polisi Mkoa wa Tarime/ Rorya wamekamata malori saba ya sukari yaliyobeba tani 93.70, kutokana na operesheni ya kupambana na magendo iliyoshamiri ya uvushaji sukari kwenda Kenya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tarime/Rorya, Deusdedit Kato, alisema walikamata mifuko 49 yenye ujazo wa kilo 50 kila mmoja nyumbani kwa mkazi wa Sirari. Alisema tani 2.45 zilitoka Tarime na tani 91.25 Musoma.

Kato alisema kwenye ukamataji walibaini mbinu ya kuhamisha sukari kutoka kwenye mifuko yake ya asili na kuwekwa mifuko mingine, ambayo ilikamatwa ikiwa tupu ya Kampuni ya Sukari Kilombero, huku sukari ikiwa imeondolewa.

Alisema sukari hiyo ilikuwa imejazwa upya kwenye mifuko ya South Nyanza Sugar ya Kenya na kwamba, shughuli hiyo hufanyika nchini na nje ya mpaka wa Tanzania, ili isafirishwe kwa urahisi kwenda Kenya.

Kato alisema maghala mengi yaliyopekuliwa hayakuwa na sukari, inasadikiwa yameficha bidhaa hiyo baada ya kutangazwa operesheni na kuongeza kuwa, imebainika sukari ya Tanzania huingizwa Kenya kwa ushirikiano wa wahalifu wengine kutoka Kenya.

“Kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola na taarifa za kiintelijensia, tumeendesha operesheni hii kwa kukagua maghala yote na kuwahoji wahusika. Pia, tumeongeza doria kwenye njia zote za panya na halali, tumekamata mifuko ya sukari mingine ni ya hapa Tarime na malori mengine yamekamatiwa Musoma wakidai kuwa walikuwa wanakuja kuuza Tarime," alisema