Sunday, May 13, 2012

Magari ya kifahari bado yamtoa udenda Cristiano Ronaldo, ayajaza manane uani kwake


Kuwa mwanasoka ghali duniani kunafanya pesa lisiwe tatizo lako la msingi. Ni kama ilivyo kwa staa wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo. Tajiri huyu kijana ananunua chochote anachojisikia kwa sasa.

                              

Kwa mujibu wa mkataba wake, Ronaldo, analipwa kiasi cha Euro 12 milioni kwa mwaka na Real Madrid. Hii ni achilia mbali mikataba mbalimbali ya kibiashara ambayo inamwingizia mabilioni ya pesa yanayomfanya awe miongoni mwa wanasoka wanaoingiza pesa nyingi zaidi duniani kwa sasa.
Hata hivyo, ugonjwa wake wa kupenda magari ya kifahari umemfanya Ronaldo ajaze magari mengi ya bei mbaya uani kwake. Amekuwa akiyatumia mara kwenda mazoezini na katika matembezi binafsi.
Yafuatayo ni magari manane ya kifahari ambayo Ronaldo ameyajaza uani na ambayo huwa anayaendesha mara kwa mara.
                              

Bugatti Veyron
Hili ndilo gari kipenzi la Ronaldo. Bugatti Veyron ni ghali zaidi na lina mwendo wa kasi zaidi duniani. Mwendo Kasi wake wa juu huwa unafikia kilomita 407 kwa saa na linaweza kumpita dereva wa formula one anayeendesha kwa kilomita 360. Staa wa Cameroon, Samuel Eto’o ni mchezaji mwingine anayemiliki gari la aina hiyo.
Bugatti huwa linauzwa kwa oda maalumu kutoka kiwandani na mhusika analazimika kulisubiri kwa kipindi fulani wakati likitengenezwa. Linauzwa kiasi cha dola 1.2 milioni na hivyo kulifanya kuwa gari ghali zaidi duniani kwa sasa.
                              

Rolls-Royce Phantom Drophead Coupe
Rolls-Royce ni gari linaloheshimika zaidi Uingereza. Gari hili linamilikiwa na watu matajiri. Kuna watu wachache sana wanaomiliki gari hili Uingereza. Lina thamani ya dola 443,000 za Marekani.
Kinachoshangaza ni kwamba nyuma ya gari hili unaweza kufungua katika sehemu ya mizigo na kupata eneo la kukaa kufanya pikiniki.
Ukifungua kuna meza inajipandisha na kuna sehemu za kuwekea vinywaji mbalimbali.
                                

Porsche Cayenne Diesel
Gari hili limetoka Mei mwaka huu na Ronaldo alilisubiri kwa muda mrefu kulinunua moja kwa moja. Lina injini yenye nguvu na kasi yake ni kilomita 218 kwa saa. Kwa suala la mafuta, gari hili lina uwezo wa kutumia lita 10 kwa mwendo wa kilomita 100. Hili ni moja kati ya magari ya bei rahisi ambayo Ronaldo anayo. Lilimgharimu kiasi cha Euro 49,000.

                               

BMW M6
Duniani kote gari hili linatambulika kuwa ndoto ya kila mtu anayetaka kuendesha ‘Sports Car’. Kwa Ronaldo, hili ndilo gari linalomfaa zaidi kwa sababu yeye ni mwanamichezo wa hali ya juu.
Ingawa bei yake ni dola 100,000, Ronaldo hakuona shida kulinunua na kulitupia uani kwake. Ni moja kati ya magari anayotumia sana.

                                  

Porsche 911
Ni moja kati ya magari ya kifahari duniani kote. Lilimgharimu Ronaldo kiasi cha euro 201, 682 kuliweka uani kwake. Ni moja kati ya magari anayoyatumia mara kwa mara pia akienda katika starehe zake.

                                 

Bentley Continental GT
Hili ni moja kati ya magari yenye nguvu ambayo kampuni ya Bentley imewahi kuyatengeneza. Gari hili pia lina kasi kubwa huku likitumia mwendo wa kilomita 320 kwa saa. Kutokana na mapenzi yake kwa gari hili, Ronaldo alilazimika kutumia kiasi cha dola 375,000 za Marekani kwa ajili ya kulinunua na kuliweka uani kwake. Ni gari la kifahari ambalo ni ndoto ya wengi.

                                   

                                 

Ferrari F430
Gari hili la siti za watu wawili tu. Kwa sasa ndiyo dili na   Ronaldo bado ana mapenzi nalo ya dhati.
Kuna watu wanasema lishastaafishwa lakini Ronaldo hakutaka kuliuza na mpaka leo amekuwa akilitumia mara nyingi. Alitumia kitita cha dola 188,000 za Marekani kulinunua.





Audi R8
Moja kati ya magari yenye kasi duniani. Gari hili lina uwezo wa kukimbia kwa kilomita 316 kwa saa. Kwa kuliweka uwani kwake kukamilisha idadi ya magari manane ya kifahari aliyonayo, Ronaldo alilazimika kujikamua kiasi cha dola za Marekani 109,000 ili kulinunua.

Tajiri anayeishi na Papa nyumbani kwake


                                         

Bill Gates anashika nafasi ya pili katika orodha ya watu matajiri duniani. Hiyo ni kutokana na biashara yake ya kompyuta na vipuli vyake.
Anayeshika namba moja kwa utajiri duniani ni raia wa Mexico, Carlos Slim.
Gates ambaye ni Mmarekani, jina lake ni William Henry "Bill" Gates III. Alizaliwa Oktoba 28, 1955 mjini Washington, Marekani.
Ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Microsoft ambayo aliianzisha na tajiri mwenzake, Paul Allen, mwaka 1975.
Microsoft ni kampuni yenye makao yake makuu huko  Redmond, Washington, Marekani na inajishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa kompyuta na vipuli vyake duniani.
Pamoja na utajiri wake, Gates pia ni mdau mkubwa wa michezo akijihusisha na soka, gofu na tenisi.
Kupitia mfuko wake wa Bill & Belinda Foundation anashirikiana na klabu ya Barcelona ya Hispania katika kuendesha kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa polio duniani.
Kutokana na shughuli zake mbalimbali, Bill Gates ana utajiri wa Dola 61.3 bilioni (Sh5 trilioni za Kenya). Ni kati ya mabilionea wachache duniani.
Ana nyumba sehemu mbalimbali duniani lakini anaishi katika nyumba ya aina yake iliyoko katika eneo la Medina jijini Washington na liko karibu kabisa na ziwa.



                                      




Nyumba hiyo yenye vyumba vinane vya kulala,  ina thamani ya Dola 125 milioni (Sh10.2 bilioni za Kenya) na imepakana na Ziwa Washington.
James Cutler ndiye alibuni nyumba hiyo kwa kutumia mfumo wa kompyuta na aliijenga kwa kupasua mlima ulio karibu na Ziwa Washington.

                                    

Pia amejenga bwawa la samaki chini ya nyumba na limefunikwa na vioo madhubuti. Miongoni mwa samaki waliomo kwenye bwawa hilo ni pamoja na papa ambao hupita na kuonekana katika sebule ya Gates.
                                    

Gates pia ana bwawa la kuogelea kwenye nyumba yake. Bwawa hilo limefungwa vyombo vya muziki na pale mtu anapoogelea basi huburudika na muziki laini pia.
Pia mtu akiingia kwenye chumba chochote cha nyumba hiyo, taa huwaka moja kwa moja bila ya kuwashwa na mtu.
Gates ana magari kadhaa yakiwamo 1988 Porsche 959 Coupe,  1998 Lincoln Continental, 1999 Porsche 911 Convertible, Ford Focus na Limousine Chevrolet Corvette.

                                    

                                    

Pia tajiri huyo anamiliki ndege nne za kusafiria na pia ana helikopta ya kuzungukia nchini Marekani.
Miongoni mwa ndege anazomiliki Gates ni pamoja na Bombardier BD-700 Global Express ambayo bei yake ni karibu Dola 45.5 milioni.
Gates anamiliki boti yenye jina la Goygpus yenye thamani ya Dola 200 milioni .




 Tajiri huyo alimwoa Melinda French, Januari 1, 1994. Ana watoto wawili wa kike,  Jennifer Katharine Gates (1996) na Phoebe Adele (2002) na mmoja wa kiume Rory John (1999).

Nani zaidi?

Kweli kaka Kanye ameopoa mtoto wa ukweli, lakini kwangu binafsi ninapata tabu nikiangalia kati ya Kim na Amber nani mkali. Hebu angalia mwenyewe.....