Monday, April 23, 2012

Vingine vinafayika!.... Tunaelekea wapi?!Vifaa zinavyotarajia kutumika katika ujenzi wa daraja la mto Malagarasi mkoani Kigoma vikiwa vimekwama katika shirika la reli ya kati katika stesheni ya mkoa wa Morogoro (TRL) baada ya kudaiwa kushindwa kusafirishwa kwa vifaa hivyo kutokana na shirika hilo kukabiliwa na ukata wa mkoani hapo.

Vifaa zinavyotarajia kutumika katika ujenzi wa daraja la mto Malagarasi mkoani Kigoma vikiwa vimekwama katika shirika la reli ya kati katika stesheni ya mkoa wa Morogoro (TRL) baada ya kudaiwa kushindwa kusafirishwa kwa vifaa hivyo kutokana na shirika hilo kukabiliwa na ukata wa mkoani hapo.

Lulu kupanda kizimbani leo


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo itaitaja kesi ya mauaji ya msanii maarufu wa filamu nchini, Steven Kanumba inayomkabili msanii mwenzake, Elizabeth Kimemeta maarufu kama Lulu (17).
Kwa mara ya kwanza Lulu alifikishwa mahakamani hapo Aprili 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando akikabiliwa na shtaka hilo la mauaji. Alisomewa shitaka hilo na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda.
Alipofikishwa mahakamani hapo, polisi walitumia mbinu za kikachero kuwapiga chenga waandishi na kupandishwa kizimbani kisha kusomewa mashtaka katika muda usiozidi dakika 10 na baadaye kupelekwa rumande.


Moja ya mbinu zilizotumika siku hiyo ili ni kutotumia magari yenye ving'ora na ulinzi wa kutisha kama ilivyotarajiwa, badala yake walitumia magari mawili madogo.
Akimsomea hati ya mashtaka, Kaganda alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu maeneo ya Sinza Vatcan, Wilaya ya Kinondoni, Lulu alimuua, Steven Kanumba. Baada ya kumaliza kusoma shtaka hilo, Kaganda alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika. Lulu hakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina uwezo wa kuisikiliza kesi hiyo.
Hakimu Mmbando aliamuru Lulu apelekwe rumande katika Gereza la Segerea kwa sababu shtaka linalomkabili ni moja ya yale yasiyo na dhamana.