Sunday, April 22, 2012

Joseph Kony bado anaendelea kusakwa


Mwandishi Wetu, Kampala
KIKOSI maalumu cha majeshi ya Uganda bado kinaendelea kumsaka mbabe wa kivita kiongozi wa kundi la waasi la  lijulikanalo kama “Lords Resistance Army ‘ Joseph Kony.

Askari wa Kikosi Maalumu cha majeshi ya Uganda wakiwa katika operesheni maalum ya kumtafuta kiongozi wa kundi la waasi la la Uganga la Lords Resistance Army (LNRA), Joseph Kony, hivi karibuni. Picha na AFP 
Majeshi hayo yanadaiwa kuendelea kusonga mbele kwa lengo la kumsaka mbabe huyo wa kivita nchini humo aliyepo mafichoni kwa muda mrefu.
Kikosi hicho kimedaiwa kusonga mbele katika msitu mmoja mkubwa uliopo katikati ya Afrika ikiwa ni kile walichodai kumsaka kiongozi huyo.
 Kikosi hicho maalumu chenye watu 59kinachoitwa 77 ndicho kinachoongoza katika mkakati huo wa kimataifa wa kumsaka na hatimaye kumtia mbaroni Joseph Kony na wapiganaji wake waliobakia la kundi la waasi la Lords Resistance Army (LRA).
Inadaiwa kwamba Kony anaendelea kuwa mwenyeji wa misitu hiyo iliyopo katika mipaka ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR), Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambayo ni maficho yanayopendwa sana na LRA tangu kikundi hicho kilipokimbia kutoka Nchini Uganda.
“tutahakikisha tunawakamata watu hawa ma kuwarudisha nyumbani, ingawa ni kazi ngumu sana “alisema mmoja kati ya wanajeshi wa kikosi hicho maalumu.
Wanajeshi hao wanaimani kabisa kwamba Kony na kundi lake hilo la kihalifu bado wanaishi msituni kwa muda wote huo, huku wakiendelea kuwateka watoto na kuwatumia katika kundi hilo.
Pia wanadai kwamba chakula wanachokula ni viazi mwitu, pamoja na mifugo ambayo wamesema ni ya wizi huku wakinywa maji ya mito.

Wake wa zuma wahudhuria harusi


Mwandishi Wetu, Afrika Kusini
Hatimaye Rais wa Afrika Kusini  Jacob Zuma ametimiza ahadi yake ya kuongeza mke mwingine.
Wake zake wengine walihudhuria sherehe hiyo ambayo iltawaliwa na nyimbo za kijadi.
Rais huyo alivalia mavazi ya kijadi katika harusi hiyo iliyofana iliyofanyika nchini humo katika Jimbo la Kwazulu-Natal
Zuma mwenye umri wa miaka 70, alivaa ngozi ya chui na kubeba mkuki na ngao, mavazi ya jadi ya Kizulu, kwenye harusi iliyofanywa Jimbo la Kwazulu-Natal.
Kabla ya kuoa mke wake huyo inadaiwa kwamba bibi harusi huyo alikuwa  Bongi Ngema, alikuwa anapata fursa ya kufuatana na Rais Zuma kwenye ziara zake rasmi kwa miaka kadha. 

Kwe Tutafika namna hii?? Hata aibu? Mnaipeleka wapi taaluma hii?!


Haya ndio magazeti yetu... Sishangai lakini, mtu amekung;uta zero yake nzuri halafu anajipiga msasa miezi mitatu, unadhani ataandika nini zaidi!?