Monday, May 14, 2012

Baada ya kazi kubwa sasa ni kusherehekea kwa kwenda mbeleee!

 Wachzaji wa Manchester City wakishangilia baada ya kukabidhiwa Kombe la Ligi Kuu England
Wachzaji wa Manchester City wakipita mtaani jana Jumapili usiku baada ya mechi yao ya fainali iliyopelekea kupata ushindi wa Ligi Kuu England  baada ya kuifunga Queens Park Rangers.



Baada ya miaka 50 ya Uhuru

Wanafunzi wa darasa la sita wa Shule ya Msingi, Selous iliyopo wilayani Namtumbo, mkoani Ruvuma wakiendelea na masomo shuleni hapo. Picha na Mpigapicha Maalum       

Umewahi kuiona hii??!! Hakunaga!

Ndege aina ya Q400 NextGen kutoka Kampuni ya Bombardier ya Canada ikiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa   Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam jana, ikitafuta wateja wa kuikodisha au kuinunua. 

Tamwa yawapa somo wakuu wapya wa Wilaya


Shakila Nyerere
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(Tamwa), kimewataka Wakuu wa Wilaya walioteuliwa kuwa makini katika ufuatiliaji wa Watendaji wa Halmashauri katika shule za kata kuepukanana mimba na kufeli kwa wanafunzi wa kike nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Tamwa, Ananilea Nkya alisema wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wawe ni mifano kwa viongozi wengine walioko madarakani kufuatilia majukumu yanayozikabili jamii.
Alisema kwa takwimu walizozifanya kwa kushirikiana na wanahabari kupata takwimu hizo zilizohusu shule za kata katika mikoa 20 Bara na Visiwani kwa kila Wilaya moja katika Kata mbalimbali kwa shule 7 hadi 10 walibaini kuwa idadi kubwa ya wanafunzi wanoacha shule au kufeli ni wanafunzi wa kike.
Nkya alisema mazingira ya shule zilikojengwa ni hatari kutokana na kukosekana kwa mahitaji muhimu kwa wanafunzi kama vile Maji, miundombinu mibovu ya barabara  ni sababu mojawapo ya kuwapa vishawishi wanafunzi wa kike kuishi wakidanganyika kwa kupitia udhaifu wa maisha waliyonayo.

Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA), Ananilea Nkya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaamjana, wakati akitoa taarifa ya utafiti wa vyanzo vya ongezeko la wanafuzi kufeli mitihani ya Kitaifa.

“Wakati mwingine wanafunzi wa kike hulazimika kuishi kwa Walimu wa kiume na kuwa na mahusiano ya kimapenzi kinyume na maadili na sheria na wengine hujikuta wakiishi kwa vijana walioko mitaani kwa kutaka kujikimu kimaisha na kupata mahitaji ya kujikidhi wanapokuwa shuleni, hiyo yote ni hali za shule za kata kuwa na mapungufumengi,” alisema Nkya.
Nkya aliongeza kwa kusema mazingira ya shule za kata zilizoko mikoani na wilayani kwa upande wa walimu ni matatizo makubwa sana maana inafikiwa wakati mwingine shule yenye kidato cha kwanza hadi cha sita kuwa na walimu watatu ikiwa mwalimu wa somo la sayansi ni mmoja na kwingineko hakuna kabisa mwalimu wa somo hilo  la sayansi.
Walimu walioko wanaofundisha somo la sayansi ni mwalimu wa somo la sanaa ndiye anayefundisha sayansi kataka shule hizo.
“Ili taaluma ikue nchini hapa kinachotakiwa ni kuboresha mahitaji muhimu ikiwemo miundombinu kwa walimu na wanafunzi ikiwa ni pamoja na uwajibikaji wa viongozi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kufuatilia watendaji katika idara zao.”
Aliongeza kwa kusema wanafunzi wa kike hufeli na kukatiza masomo kwa kubeba mimba shuleni ni pamoja na kukosekana kwa walimu ambao kwa asilimia 80 wamekuwa wakishindwa kuwasili katika vituo vya kazi wanavyokuwa wamepangiwa wakikumbana na mazingira magumu kwa mara ya kwanza. 


Pale ubora unapoonekana


Mkurugenzi wa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma, akimkabidhi Laptop Zaitun Kaijage (kulia, amabaye ni mmoja kati ya washindi wa tuzo za masomo ya fani ya teknolojia ya mawasiliano katika mamlaka hiyo, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi.