Sunday, February 12, 2012

Hii ni hatari

Watoto wakazi wa Kivule Bombambili, Manispaa ya Ilala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakivuka mto kwa kupita juu ya gogo la mnazi. Mvua zilizonyesha mwishoni wa mwaka jana zilisababisha mafuriko yaliyosomba karavati katika eneo na kusababisha kwa sasa wananchi kwa shida na ni hatari.

Ukuta aliojengwa kuzuia maji ya Bahari ya Hindi yasiharibu kingo za eneo la Ocean Road jijini Dar es Salaam, umebomoka kutokana na mawimbi ya bahari hiyo kuongeza kasi inayochangiwa na mabadiliko ya tabia nchi duniani. Hali hiyo inatishia mazingira ya eneo hilo.

Kazi ni kazi, usidharau ya mwenzako

Mchuuzi wa dagaa, Mohammed Maulid, akianika bidhaa hiyo baada ya kuvuliwa Bahari ya Hindi, Dar es Salaam jana, ikiwa ni maandalizi ya kuwakaanga tayari kuwapeleka kwa wateja Kata ya Msanga, wilayani Kisarawe, mkoani Pwani.

Fundi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), akipanda kwenye nguzo ya umeme tayari kwa kufunga nyaya ili kusambaza umeme kwenye eneo la Mabwepande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam walikohamishiwa waathirika wa mafuriko yaliyotokea mwishoni mwa Desemba mwaka jana.