Sunday, November 27, 2011

Congo yachafuka, wawili wauawa


Ikiwa leo wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanatarajia kumchagua rais wao vurugu kubwa zaendelea kushika kasi katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.

Kampeni hizo ambazo hazikumaliza katika muda uliokusudiwa na tume ya uchaguzi lakini kutokana na vurugu kubwa ambazo mpaka sasa zimesababisha watu wawili kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Juzi, polisi nchini humo ilipiga marufuku kampeni zote za uchaguzi katika mji mkuu Kinshasa baada ya wafuasi wa chama tawala na upinzani kushambuliana na kusababisha mauaji.

Licha ya vurugu hizo kuendelea nchini humo na kusababisha wananchi kuwa na wasiwasi zaidi hasa leo ambapo wanamchagua rais wao atakaoliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine pamoja na wabunge.


Wafuasi wa chama kikuu cha upinzani cha UDPS katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakiyakimbia mabomu ya machozi yaliyolipuliwa na polisi nchini humo karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa uliopo mjini Kinshasa.

Rais Joseph Kabila na mahasimu wake wakuu wawili Etienne Tshisekedi na Vital Kamerhe juzi walikuwa wamejitayarisha kufanya kampeni za lala salama za uchaguzi huo katika maeneo yanayokaribiana mjini Kinshasa hata hivyo kampeni hizo zilikatishwa na vurugu kubwa zilizoibuka mkutanoni hapo.

Habari zinasema, licha ya leo wananchi wanamchagua kiongozi wao lakini bado kuna wasiwasi kuhusu ugawaji karatasi za kupigia kura, kwa kuwa ndege zimeshindwa kufika baadhi ya maeneo kutokana na hali mbaya ya hewa.


Hivi tunaelekea wapi??!!