Tuesday, April 10, 2012

Hatimaye Steven Kanumba apumzishwa katika nyumba yake ya milele

















Mayowe yalianza, vilio kila kona baada ya jeneza lenye mwili wa marehemu kuingia katika Viwanja vya Leaders Club




Waombolezaji walishindwa kuzuia hisia zao






















Wema, Aut nao walikuwapo kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu.








Irene Uwoya akipatiwa matibabu baada ya kuzimia


Ukawa ni mwendo wa watu kuzimia tu











Hapa makaburini kuna umati mkubwa wa watu ambao haujapata kutokea. Jua ni kali sana. Hata hivyo, shughuli ya mazishi inaonekana kuendelea. Kuna waliokaa vivulini. Kuna waliopanda juu ya miti. Kuna waliopanda ukutani. Kulikuwa hakuna hata pa kupitia





Hapa makaburini hakuna aliye na wakati wa kuokota kandambili yake iliyokatika au kuvuka miguuni, nyingi zimelowana matope. Ajabu ya tope hili, sijui limetoka wapi wakati kuna jua kali linalokausha vichwa vya watu.


Hatimaye mdogo wetu akalazwa katika nyumba yake ya milele, sasa ndio tunaamini kuwa hatutomwona tena mpendwa wetu Steven Kanumba, ulale pema peponi... Amin