Sunday, September 18, 2011

Mendes kwenye mapenzi


Kuna taarifa kuwa wakali wa filamu, Ryan Gosling na Eva Mendes ni wapenzi.
Gosling na Mendes walinaswa na paparazzi wakiwa katika mkao ulioashiria walikuwa wapenzi.
Mastaa hao kwa sasa wako katika matayarisho ya filamu ya "The Place Beyond the Pines".
Habari hiyo inathibitisha sasa habari iliyotolewa na gazeti la Us Weekly hivi karibuni.
Pia gazeti hilo lilitoa picha ya watu hao wakiwa wameshikana mikono na kukumbatiana wakati walipotembelea Disneyland mjini Anaheim, Marekani.

Milian amzingua P.Diddy


Kivazi cha mkali wa filamu na muziki, Christina Milian kiliwaacha watu hoi waliohudhuria pati iliyoandaliwa na P.Diddy.
Christina aliyeng'ara karika filamu ya ìGhost of Girlfriends Pastî, alifika katika sherehe hiyo akiwa amevaa kaptura fupi, sidiria ya bikini na viatu virefu.
P.Diddy aliandaa pati hiyo katika klabu ya Palms Casino Resort huko Las Vegas, wikiendi iliyopita.
P.Diddy ni kati ya watu waliomsifia kimwana huyo na hata kufikia kuandika kwenye mtandao wa Twitter kuwa Christina ni moto wa kuotea mbali.

Mume wa J.Lo alonga


Miezi miwili baada ya kuachana, mume wa Jennifer Lopez, ameanika kilichosababisha kuvunjika kwa ndoa hiyo.
Marc Anthony alizungumza na televisheni ya ABC News, akidai kazi ndio ziliwafanya washindwe kuishi pamoja.
Anthony alikanusha vikali kuwa alikuwa anamnyanyasa Jennifer, ambaye ni maarufu kwa jina la J.Lo.
Mume alishikilia kuwa alikuwa bado anampenda J.Lo ila masuala ya kuwa bize ndio yaliwagonganisha.
Baada ya kuvunjika kwa ndoa hiyo, watu hao waliamua kukaa kimya.
J.Lo katika siku za karibuni amekuwa bize na kipindi cha kusaka vipaji cha American Idol.

Mtoto wa Beyonce azua mjadala


Kitendo cha Beyonce kutangaza kuwa ni mja mzito, kimezua mjadala wa jinsia ya mtoto huyo katika mitandao ya mawasiliano ya Twitter na Facebook.
Wadau wameanza kujiuliza kuwa Beyonce, ambaye atazaa na mumewe Jay-Z, atapata mtoto gani wa kwanza.
Pia watu wameanza kujiuliza kuwa mwanamuziki huyo atajifungulia wapi mtoto huyo.
Mashabiki wa watu hao wanajadili pia kama mtoto huyo ataingia katika masuala ya muziki.
Mtoto anatokana na mwanamuziki, Beyonce, ambaye ni mkali wa R&B wakati Jay Z ni rapa mahiri.

Kobe Bryant ajifananisha na nyoka





Kobe Bean Bryant ni nyota wa mpira wa kikapu, ambaye anachezea Los Angeles inayoshiriki Ligi ya Marekani (NBA).
Bryant, ambaye amezaliwa Agosti 23, 1978), ndio mfungaji mahiri wa timu hiyo.
Anajiita mwenyewe jina utani la "Black Mamba", akijifananisha na nyoka huyo, ambaye anapatikana barani Afrika.
Nyoka huyo yupo katika nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Sudan, Ethiopia, Eritrea, Somalia, Kenya, Uganda, Tanzania, Msumbiji, Swaziland, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Botswana, Afrika Kusini na Namibia.
Kobe anajifananisha na nyoka huyo kwa kuwa naye ana shabaha kubwa ya kufunga na kasi.
Nyoka aina ya Black Mamba husifika kwa kuteleza kwa kasi na kushambulia bila ya kukosea.
Black Mamba anaaminika kuwa ndio nyoka mwenye kasi zaidi duniani kutokana na uwezo wa kukimbia kilomita 20 kwa saa.
Ukiangalia na rekodi ya Kobe utagundua hajafanya makosa kujilinganisha na nyoka huyo kwani anashikilia rekodi ya kuifungia pointi nyingi zaidi Lakers.
Pia ni mtu wa pili kufunga pointi nyingi zaidi katika mchezo mmoja wa NBA. Amewahi kufunga pointi 81. Wilt Chamberlain ndio anashikilia rekodi kwa kufunga pointi 100 katika mechi moja, aliyoweka mwaka 1962.
Kobe pia ni miongoni mwa watu watatu waliofunga pointi nyingi zaidi katika historia ya NBA.
Ana utajiri wa kiasi cha Dola 200 milioni (Sh. 18 bilioni za Kenya) ukitokana na mshahara wake na matangazo mbalimbali ya biashara.
Mshahara wake wa mwaka katika timu yake ya Lakers ni kiasi cha Dola 24 milioni (Sh. 2.2 bilioni za Kenya)
Ana mkataba wa matangazo na kampuni ya kutengeza vifaa vya michezo ya Nike. Pia ana mikataba na makampuni ya Coca-Cola, McDonald, NBA Infusion Ball, Upper Deck, Ferrero SpA na Russell Corporation.
Bryant pia ana mkataba wa matangazo na Shirika la Ndege la Uturuki.
Pia anafanya matangazo ya magari ya Mercedez Benz nchini China.
Kobe pia anafanya muziki, na hivi karibuni alishirikiana na mwanamuziki wa Taiwan, Jay Chou kutengeneza wimbo wa "The Heaven and Earth Challenge".
Fedha zitakazotokana na wimbo huo zitasambazwa duniani kote kwa ajili ya kutengeneza viwanja vya mpira wa kikapu.
Bryant na mkewe Vanessa wana nyumba ya thamani ya Dola 4 milioni (Sh. 375 milioni za Kenya) huko Newport Beach, Marekani.
Pia alinunua nyumba nyingine ya thamani ya Dola 13.5 milioni (Sh. 1.2 bilioni za Kenya)iliyoko Newport pia, katika Jimbo la California. Nyumba hiyo ipo katika ufukwe wa bahari kwenye eneo hilo.

Nyumba hiyo ina vyumba sita vya kulala, mabafu 11 ya kuogea, bwawa la kuogelea na gereji yenye uwezo wa kuingiza magari matano.
Bryant pia ana nyumba nyingine katika jiji la Los Angeles.
Pia ana magari aina ya Range Rover, Ferrari F430, 360 Modena, 612 Scaglietti, Bentley Continental GT, Azure Mulliner, Cadillac Escalade na 1963 Chevrolet Impala.





Kobe pia anamiliki ndege yake, ambayo hutembea nayo sehemu mbalimbali duniani.
Alianzia mpira wa kikapu katika shule ya Lower Merion kabla ya kusajiliwa na Charlotte Hornets mwaka 1996.
Alikaa kwa muda mfupi kabla ya kuchukuliwa na Los Angeles Lakers, ambako yuko hadi sasa.
Kobe amepata tuzo nyingi za NBA, ikiwamo mchezaji bora mwaka 2003, kuchezea timu ya nyota wa michuano hiyo mara 13 na medali ya dhahabu ya Olimpiki mwaka 2008.
Ni mtoto wa kocha wa zamani wa Los Angeles Sparks, Joe "Jellybean" Bryant na mama yake anaitwa Pamela Cox Bryant.
Yeye na mkewe Vanessa wana watoto wawili wa kike.

Miss Universe:Sitakuwa bishoo


Leila Lopes, ambaye ni msichana wa kwanza wa Angola kushinda taji la Miss Universe, ameahidi kusaidia watu masikini nchi mwake.
Alidai kuwa taji hilo halitamfanya aanze kuringa na kujisikia bishoo.
Mlimbwende huyo mwenye umri wa miaka 25, alisema mara zote amekuwa na huruma na watu wenye matatizo.
ìNikiwa na taji la Miss Angola nimekuwa nikisaidia watoto wa mitaani na wale wenye ugonjwa wa Ukimwi.î
Leila alieleza mradi wake unaofuata ni kusaidia wazee, ambao wanashindwa kujikimu.
ìKwa kweli sitabadilika hata baada ya kushinda taji hili kubwa. Watu wanafikiri pengine nitaanza kujisikia. Hapana haitatokea,î aliongeza Leila, baada ya kutangazwa mshindi wa taji hilo wiki hii.

J.Lo aibua na mpenzi mpya


Baada ya kuachana na Marc Anthony, mwanamuziki Jennifer Lopez amepata mpenzi mpya.
Lopez maarufu kwa jina la J.Lo hivi karibuni, alionekana na Bradley Cooper.


"Wana uhusiano wa mapenzi," alidokeza mtu mmoja, ambaye yuko karibu na J.Lo.
Baada ya habari hiyo, paparazi walifuatilia na kuwanasa katika mgawaha mmoja jijini New York.
Lopez alikuwa amevaa gauni jeupe na mara nyingi alikuwa akimkumbatia Cooper.
Lopez aliachana na Anthony hivi karibuni baada ya kuishi kwenye ndoa kwa miaka saba.

Angelina Jolie amtibulia Jennifer


Wakati Brad Pitt alipomwacha Jennifer Aniston na kumchukua Angelina Jolie, miaka sita iliyopita kulisababisha bifu huko Hollywood, Marekani.
Angelina na Jennifer mara nyingi wamekuwa wakitupiana vijembe kwenye mahojiano kuhusiana na Brad Pitt.

Jolie
Jenifer
Jennifer sasa amepata mpenzi mpya Justin Theroux na wamepanga kufunga ndoa mwakani.
Angelina, hata hivyo, amepanga kumvurugia Jennifer kwani amepanga kufunga ndoa na Brad mwakani pia.
Inasemekana Angelina anataka kumuwahi Jennifer kwa kuwa wa kwanza kufunga ndoa.
Brad inasemekana pia ameunga mkono wazo la Jennifer la kufunga ndoa.

Wes Brown achanganya soka na biashara



Wes Brown ni beki wa timu ya Sunderland inayoshiriki Ligi Kuu England, mwenye sifa ya kucheza nafasi zote za ulinzi.
Kwa muda mrefu alikuwa akichezea Manchester United lakini msimu huu amejiunga na Sunderland.
Brown ana utajiri unaokadiriwa kuwa pauni milioni 10 (Sh. 25 bilioni) ukitokana na kucheza soka na shughuli zake mbalimbali za biashara.
Ana kampuni inayoitwa Wes Brown Company, ambayo ndio inasimamia shughuli zake mbalimbali. Shughuli zake ni kama za masoko na matangazo.
Kampuni hiyo ina mali zisizohamishika zenye thamani ya pauni 598,000 (Sh. 1.5 bilioni).
Brown inasemekana anapata kiasi cha pauni 50,000 (Sh. 127 milioni) kwa wiki katika klabu yake mpya ya Sunderland.
Beki huyo anamiliki jumba lenye thamani ya pauni 4.5 milioni (Sh. 1.4 bilioni) huko Cheshire.
Jumba lenye vyumba vitano vya kulala lina chumba kikubwa kwa ajili ya kuangalia sinema, bwawa la kuogelea na studio.


Pia lina jiko la aina yake na sehemu kubwa ya uwanja, ambao kuna wakati Wes alikuwa akicheza gofu.
Wes pia ni mpenzi wa magari, na anayomiliki ni pamoja na BMW X5, Audi, Aston, Martin, Porsche, Mercedes Benz na Hummer 2.







Brown amezaliwa Oktoba 13, 1979 na alianzia soka yake katika timu ya yosso ya Manchester United mwaka 1996.
Alisajiliwa katika timu ya wakubwa mwaka 1998 na kupata nafasi katika kikosi cha kwanza katika msimu wa 1998ñ99.
Brown pia alinga'ra katika msimu wa 2000 na katika kipindi cha miaka nane ameshinda mataji mbalimbali.
Alishinda mataji ya ubingwa wa England, Kombe la FA, Kombe la Ligi na Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Brown aliitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha England mwaka 1999 na alikuwemo kwenye kikosi cha Kombe la Dunia mwaka 2002.
Alicheza michuano ya awali ya Euro 2008 lakini England haikufuzu kwa fainali hizo.
Brown aliachana na timu ya England, Agosti 8, 2010, ikiwa siku moja baada ya kuitwa kwenye kikosi na kocha Fabio Capello.
Brown ameoana na Leanne Wassell, ambaye wanaishi naye Alderley Edge, Cheshire. Wana watoto wawili Halle na Lilia.

Angalia mambo haya, ukistaajabu ya...................!!!




Cheki utamu wa maziwa fresh!... Dogo mpaka kapandwa na mdadi