Tuesday, June 19, 2012

Safari ya Drogba China yaiva



Add caption
Didier Drogba kazini

SHANGHAI, China
SAFARI ya mshambuliaji wa zamani wa Chelsea ya England, Didier Drogba kwenda kumalizia soka nchini China, imeiva na anatarajia kujiunga na timu ya Shanghai Shenhua wakati wowote wiki hii.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast ameelezwa kuingia mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya pauni 25 milioni (sawa na Sh60.8 Bilioni).
Kwa sasa Drogba (34) yuko nchini India
Kwa mujibu wa bosi wa klabu hiyo ya China, Zhu Jun, Drogba anatarajia kutangaza uhamisho huo kwenye tovuti yake binafsi.
Mbali na timu hiyo ya China kumtaka drogba, klabu nyingine tajiri ya falme za Kiarabu, Al Wasl FC nayo imeonyesha nia.
safari yake ya China inatarajia kumkutanisha na mshambuliaji mwenzake aliyecheza naye pamoja kwenye kikosi cha Chelsea, Nicolas Anelka.
"Hatua inayofuata kwangu nimefurahi," alisema Drogba wakati wa ziara yake nchini India.
"Muda siyo mrefu nitatangaza uamuzi wangu, lakini kwa sasa ningependa msubiri kwanza," alisema Drogba.
Klabu hiyo ya China imekusudia kufanya mageuzi makubwa kwa kusajili wachezaji wengi wa kigeni pamoja na kocha pia.

Ilimtimua Kocha Jean Tigana mapema mwezi huu na nafasi yake kuchukuliwa na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Argentina, Sergio Batista.