Tuesday, July 31, 2012

Tanesco waendeleza libeneke na wezi wa umeme

Mtuhumiwa wa wizi wa umeme Jeilan Mohamed, akiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi huku akiangalia mafundi wanavyong’oa mita ya umeme kwenye nyumba yake Buguruni Malapa Jijini Dar es Salaam jana kwenye zoezi linaloendelea la kukamata wezi.

Fundi Mwandamizi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tenesco)  Didas Lwinga, akiwaonyesha waandishi wa habari mita iliyofunguliwa na kubandikwa gundi (Super Glue) mara baada ya kuing’oa.


Mtuhumiwa wa wizi wa umeme Jeilan Mohamed, akiongozwa na jeshi la polisi kupanda gari baada ya kutuhumiwakuliibia umeme kwa njia ya kuunganisha kabla haujafika kwenye mita  maeneo ya Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam.