Sunday, October 30, 2011

Sijaelewa vizuri, ama sijui!

Inakuwaje unapiga simu haipokelewi, wewe unaendelea kupiga! Kwa nini ung'ang'anie kupiga simu wakati umekwishapiga mara ya kwanza haijapokelewa, unaendelea kupiga zaidi hata ya mara tano!
Ukiona kimya ujue muhusika yupo mbali na simu, akiichukua simu yake ataona kuwa alipigiwa na atakupigia, tusing'ang'anie kupiga jamani, pengine mwenyewe amelala au yupo busy

Mtoto wa Nguema Mbasogo aanza kufilisiwa


Wakati wa kutawala maisha yote hauna nafasi tena. Upepo wa mabadiliko uliovuma na kuwang'oa vigogo waliotawala kwa miaka mingi Afrika, sasa unaonekana kunaelekea kwa kiongozi mwingine barani Afrika aliyekaa madarakani kwa muda mrefu.

Upepo wa mabadiliko sasa unaelekea nchini Equatoral Guinea ambako mtoto wa rais wa nchi hiyo ambaye anatarajwa kuwa mrithi wa nchi atakapo ondoka madarakani baba yake iwe kustaafu au kifo, ameanza kuandamwa na mataifa mbalimbali wakitaka afilisiwe huku wakimwita ‘mla rushwa.’

Kilichomkuta Gaddafi chaweza kumkuta mtoto huyo, Teodoro Nguema Obiang Mangue kwa sababu nguvu kubwa ya kumuondoa madarakani inatoka nchi za magharibi.

Mangue anatuhumiwa kutumia madaraka yake na ya baba yake kujipatia kipato isivyo halali.

Mangue ni Waziri wa Kilimo na Misitu, anatuhumiwa kuwa na mali nyingi nje ya nchi ambazo zimekubaliana kuzishikilia mali hizo na kuzirudisha kwa wananchi itakapobidi.

Ufaransa yakamata magari yake

Wakati watu 'wakimechisha' viatu na nguo, Mangue anasifika kwa kununua viatu na magari yanayofanana. Akivaa vitu vya bluu, atatoka na Ferrari Enzo ya rangi hiyo.


Ufaranza imekuwa ya kwanza kumchukulia hatua kwa kuyakamata magari yake yote ya kifahari aliyokuwa akiyamili katika ardhi ya nchi hiyo.

Miongoni mwa magari ya kifahari yaliyokamatwa ni pamoja 'Bugatti Veyrons', 'Maserati MC12', 'Porsche Carrera GT', 'Ferrari Enzo', Aston Martin,Rolls Royce Phantom coupé na 'Ferrari 599 GTO'.

Magari yote yaliyokuwa katika ardhi ya nchi hiyo yanashikiliwa ingawa haijajulikana mpaka sasa yatapelekwa nchini Equatorial Guinea au yatauzwa na pesa hizo kurudishwa.

Hata hivyo, nchi hii imeilaumu Serikali ya Marekani kwa kushindwa kulizuia jumba la kifahari la mwanamume huyo lililopo eneo la Malibu ambalo linasifika kwa kuishi mastaa wenye pesa wa nchi hiyo.

Mangue anamiliki jumba linalokadiriwa kuwa na thamani ya dola za Marekani milioni 35 ambalo alilinunua mwaka 2008 kwa fedha taslimu.


Mbali na jumba hilo, anamiliki ndege binafsi na boti ya kifahari hata hivyo uchunguzi wa awali wa Marekani unasema vitu hivyo amevihamisha kutoka huko na haijulikani amevipeleka nchi gani.

Anapenda umaarufu

Mangue anasifika kwa kuwa karibu na wasanii wakubwa maarufu, moja kati ya watu wake wa karibu ni Mwanamuziki, Janeth Jackson na familia nzima.


Pia anakumbukwa kwa kuinunua ‘glavu’ ya Mwanamuziki Michael Jackson kwa kiasi cha dola za Marekani 3.2milioni, pengine huu ulikuwa mwanzo wa familia ya Jackson kumjua.

Inaelezwa mara kadhaa amekua akiwaalika nchini kwao kaka wa marehemu, Michael Jackson, huku akisisitiza ujio wao ni kibiashara.

Inaelezwa kuwa pia Mangue amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii wa Marekani, Eve. Uhusiano huu ulidumu kwa muda wa miaka miwili.


Anakumbukwa kwa kumfanyia sherehe za kifahari mwanamuziki huyo na kumnunulia zawadi kubwa ikiwemo magari ya kifahari.

Yote kwa yote, Ufaransa imeanza kuchukua hatua, je, ni nchi gani inafuatia katika hili, na je, huu ni mwanzo wa mwisho wa utawala wa baba yake, Teodoro Obiang Nguema Mbasogo?


Hii ndio Bongo bwana, we acha tu!

Tuwalee, nasi ni watoto wetu

Mlezi wa watoto wa Kituo cha Watoto Yatima na wanaoishi katika Mazingira Magumu cha Samaritan, jijini Arusha, Eli Malemba, akiwanyeshwa uji watoto Ebeneza na Baraka, wanaolelewa katika kituo hicho.