Tuesday, August 23, 2011


Mtoto wa Gaddafi asema hajakamatwa, aapa atapambana hadi kieleweke!

Mtoto wa kiume wa kiongozi wa Libya, kanali Muammar Gaddafi, Seif Al Islam, amejitokeza hadharani katika hoteli moja mjini Tripoli na kukanusha madai kuwa amekamatwa.

Habari zinasema kuwa, Al Islam aliibuka katika hoteli hiyo jana asubuhi ambayo waandishi wa habari wa kigeni wamekuwa wakiishi mjini hapo na kuwaeleza waandishi hao, wananchi wa Libya na dunia kwa ujumla yupo salama na ataendeleza mapambano mpaka kieleweke.

Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), Luis Moreno-Ocampo, na waasi wa Libya walisema juzi kuwa mtoto huyo wa Gaddafi wamemkamata.

Seif amesema utawala wa Gaddafi bado unaudhibiti mji mkuu Tripoli na kwamba baba yake yuko salama na katika hali nzuri mjini humo.

Al-islam ambaye alionekana kuwa mchangamfu na mwenye shauku kuu aliongeza waasi wameingia kwenye ''mtego'' mjini Tripoli na kwamba wanajeshi wanaomuunga mkono Kanali Gaddafi walikuwa ''wamevunja uti wa mgogo wa waasi hao''.


"Niko hapa kuuondoa uwongo uliotangazwa" alisema Saif Al-Islam mbele ya kikundi cha waandishi wa habari mjini Tripoli katika kitongoji cha Bab al- Azizyah ambapo ni makao ya baba yake.

“Mji mkuu Tripoli ungali uko chini ya udhibiti wa utawala wa baba yangu na kwamba Magharibi ilitumia teknolojia yake kuvuruga mifumo ya mawasiliano na kutuma jumbe kwa wananchi kwamba utawala wa Gaddafi umeanguka,” alisema Al- Islam.


Mtoto wa kiume wa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi, Seif Al Islam akiwa na wafuasi wake pamoja na waandishi wa habari, akionyesha alama ya ushindi ya V baada ya kuibuka katika hoteli moja mjini Tripoli jana asubuhi. Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), Luis Moreno-Ocampo, na waasi wa Libya walisema juzi kuwa mtoto huyo wa Gaddafi wamemkamata.

Sunday, August 21, 2011


Mambo matano ya kuiweka juu Chelsea

Mafanikio ya Chelsea yanategemea juhudi za wachezaji mmoja mmoja na timu yote kwa ujumla.
Chelsea ina wachezaji wazuri, lakini si kila mara wachezaji hao wamekuwa wakicheza kwa kiwango kikubwa. Katika soka hicho si kitu cha ajabu, kuna wakati mchezaji anaweza kuwika na kuna wakati anaweza kushuka kiwango na kuacha watu wakiwa midomo wazi.
Vilevile kuna baadhi ya wachezaji huwa ni muhimu katika klabu zao kuliko wengine, hiyo inategemea nafasi ya mchezaji, aina ya uchezaji na kocha anampanga mara ngapi. Chelsea nayo ina wachezaji muhimu na wengine wana umuhimu wa wastani.
Makala hii inawachambua wachezaji watano wa Chelsea ambao ni ngao ya kikosi, ambao wanaweza kuchangia kupatikana kwa ubingwa msimu huu.

5. Petr Cech
Timu zote hung'aa zinapokuwa na beki wa maana. Kama timu ina kipa mzuri, hiyo ni hatua ya kwanza kuelekea katika mafanikio. Chelsea ina bahati kwa kuwa ina kipa makini, Petr Cech. Cech amekuwa mkongwa katika kikosi cha Stamford Bridge. Ameidakia Chelsea mechi zaidi ya 300 na kuna dalili kwamba ataendelea kucheza katika klabu hiyo kwa miaka kadhaa.
Cech mwenye umri wa miaka 29 anadaiwa kuwa ndio kipa mzuri zaidi katika Ligi Kuu England kwa sasa. Mchezaji huyo yupo katika kiwango cha hali ya juu, anaweza kupigana na presha zote za Ligi Kuu England na michuano mingine ya kimataifa. Kama wachezaji wa ndani wakifanya vizuri huku Cech akiboresha kiwango chake mambo yatakuwa mazuri.


4. Winga
Hapa hatajwi mchezaji yeyote kwa kuwa nafasi ya winga ya Chelsea ni nzuri. Lakini winga wa Chelsea wanatakiwa kufanya kazi ya ziada kusababisha usumbufu kutoka pembeni badala ya katikati kama walivyofanya mara kadhaa msimu uliopita.
Ikumbukwe kuwa hakuna timu inayoweza kutisha sana kama ikitegemea mipira ya kati pekee.

3. John Terry
Umri wa Terry unaweza kuwa umesonga kidogo, lakini nahodha huyo wa Chelsea anabaki kuwa mmoja wa mabeki wa kati wazuri duniani.
Chelsea inajivunia kuwa na beki huyo na amekuwa akiwaokoa katika hatari nyingi.
Mchezaji huyo ni mzuri kwa mipira ya juu na chini, ni wazi kuwa ataisaidia timu yake kufanya vizuri msimu huu.
Kama Terry akiumia au asipokuwepo uwanjani ni rahisi kuona Chelsea ikihangaika kufanya vizuri. Hiyo inaamisha kuwa uongozi wa Chelsea unatakiwa kuomba mchezaji huyo asishuke kiwango katika siku za karibuni la sivyo mambo yatakuwa magumu.

2. Frank Lampard
Watu wamekuwa wakizungumza mambo tofauti juu ya Frank Lampard, wengine wanasema ameanza kuishiwa, wengine wanasema baada ya muda mfupi ataondoka. Lakini bila kujali watu wanasema nini, ukweli ni kuwa Lampard ni mmoja kati ya wachezaji wazuri na hana dalili ya kustaafu karibuni.
Kweli, umri wake umesonga, lakini mchezaji huyo mwenye miaka 33 bado ana kiwango kikubwa. Huenda akapata shida kwenda sambamba na staili ya kocha mpya Andre Villas-Boas, lakini baada ya muda mfupi atasimama.
Tayari Lampard amejinoa vya kutosha katika mechi za kujiandaa na msimu na sasa anatakiwa kuendelea na kasi hiyo.
Lampard ni mchezaji mzuri na klabu yake inamtegemea kufanya mambo makubwa.

1. Didier Drogba/Fernando Torres
Chelsea inahitaji mabao ya kutosha.
Klabu hiyo ina washambuliaji wawili wazuri duniani lakini mmoja wao anatakiwa kuanza mara kwa mara.
Andre Villas-Boas amepanga vizuri maeneo mengine lakini linapokuja suala la washambuliaji anaonekana kuwa na wakati mgumu.
Didier Drogba na Fernando Torres wote ni wachezaji wa daraja la kwanza duniani lakini hakuna mchezaji kati yao, ambaye ameonyesha kiwango kwenye kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Watu wanaweza kusema umri wao umesonga lakini si kweli kwani Torres ana miaka 27. Kinachotokea hapo ni suala la kujiamini.
Drogba ni mchezaji mzuri lakini amekuwa akiwekwa nyuma ya Torres, na hiyo inamuondolea kujiamiani kwa kiasi fulani. Torres, ambaye alitua katika timu Januari bado hajafanya vizuri uwanjani.


Hitimisho
Kocha mpya anatakiwa kutafuta mbinu ya kuwapanga washambuliaji la sivyo hadithi yao itakuwa kama ya kocha wa zamani Carlo Ancelotti. Iwapo kocha akipata seti nzuri, kikosi kitafanya makubwa ziadi.

Vitimbi vya Mourinho vyamchefua Guardiola
Vitimbi vya kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho vimemchefua kocha wa Barcelona, Pep Guardiola.
Mourinho alikwenda kwenye benchi la ufundi la Barcelona na kuchoma kwa kidole chake kwenye jicho la kocha msaidizi wa timu hiyo wakati wa mechi kati ya timu hizo mbili, Jumatano iliyopita.
Katika pambano la Super Cup lililotawaliwa na ubabe, Real Madrid ililala 3-2 katika Uwanja wa Nou Camp.
Kwa matokeo hayo ikawa imefungwa jumla ya mabao 5-4 na Barcelona ikanyakua taji hilo. Timu hizo zilifungana 2-2 , Jumapili iliyopita kwenye mechi ya kwanza.
Beki wa Real Madrid, Marcelo alitolewa kwa kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mbaya kiungo mpya wa Barcelona, Cesc Fabregas.


Kitendo hicho kilisababisha zogo baina ya makocha wa timu hizo.
Mourinho alimfuata kocha msaidizi, Tito Vilanova na kumchoma jichoni kwa kidole na baadaye kumfanyia mzaha kama anambusu.
Guardiola alilalamika: "Kila mtu ameona kilichotokea. Kuna vitu havitakiwi kutokea katika mchezo wa soka."
"Kwa kweli tabia hizi hazipaswi kuachwa kuendelea."
Mourinho alijitetea kuwa hakufahamu nani aliyemchoma jichoni.



Lakshmi Mittal: Ana basi la ajabu
Tatiri wa India, Lakshmi Mittal ni kati ya wamiliki wa klabu ya soka ya Queens Park Rangers iliyopanda daraja msimu huu kwenye Ligi Kuu England.
Mwanahisa mkubwa mwingine kwenye klabu hiyo ni Bernie Ecclestone, ambaye ni rafiki mkubwa wa Mittal.
Ecclestone anafahamika kutokana na kumiliki haki za mbio za magari za Formula One.
Mittal, ambaye ni raia wa India, anahesabiwa kama mtu tajiri zaidi barani Asia na Uingereza.
Anashika nafasi ya sita miongoni mwa mabilionea duniani, utajiri wake ukikadiriwa kuwa Dola 31 bilioni (Sh. 2.8 trilioni za Kenya) ukitokana zaidi na mauzo ya bidhaa za chuma.
Mittal ana majumba, magari madogo, ndege, basi, helikopta na boti.
Mittal ana basi lililotengenezwa na kampuni ya kutengeneza mabasi ya Featherlite Luxury.
Basi hilo ni la kipekee likiwa na vitu vya anasa ndani yake na thamani yake ni Dola 2.5 milioni (Sh. 229 milioni za Kenya)


Ndani ya basi, sebuleni
Ndani ya basi, chumba cha kulala
Ndani ya basi, bafuni, chooni
Lina chumba cha kulala, bafu ya kuogea, chumba cha kulia chakula, sebule, jiko na saluni.
Mittal pia ana majumba sehemu mbalimbali duniani ingawa anashikilia rekodi ya kuwa na nyumba ya bei ghali zaidi duniani.
Anaishi katika jumba la thamani ya pauni 250 milioni (Sh. 37 bilioni za Kenya) katika mtaa wa Kensington Palace Gardens, jijini London, Uingereza. Aliinunua kutoka kwa Ecclestone.
Nyumba hiyo ina vyumba 12 vya kulala, bafu, ukumbi mkubwa, bwawa la kuogelea lililotengenezwa kwa madini ya dhahabu na sehemu ya kuegeshea magari 20.
Ukiachia nyumba hiyo anayoishi, pia ana nyumba mbili zaidi katika jiji la London.
Pia ana jumba la thamani ya pauni 15 milioni (Sh. 2.2 bilioni za Kenya) huko Scotland.
Pia nyumba nyingine katika mtaa wa Aurangzeb katika jiji la Delhi, nchini India.
Mittal pia ana nyumba nyingine katika nchi za Indonesia na Trinidad.
Ana magari mengi tu lakini yanayojulikana ni yale ya Ferrari, Range Rover, Mercedes Benz, Jaguar na mengineyo.




Ndani ya basi, hapa ndio salon
Pia ana boti kubwa aliyoipa jina la Amevi na pia ana ndege yake binafsi na helikopta.
Mittal, ambaye amezaliwa Juni 15, 1950, anamiliki kampuni ya ArcelorMittal, ambayo inaongoza duniani kwa kutengeneza vifaa vya bidhaa ya chuma.

Jessie J kunyoa upara
Mkali wa muziki wa pop, Jessie J amesema atanyoa upara kwa ajili ya hisani.
Jessie alieleza kuwa anataka kunyoa nywele zake nyeusi ikiwa kama njia ya kusaka fedha za kusaidia wasiojiweza.
"Nimechukua uamuzi wa kunyoa ili kukusanya fedha kusaidia watu masikini," alisema.
Jessie pia hivi karibuni alianzisha kampeni ya kusaidia vijana kusoma kwenye vyuo.
Alisema fedha atakazopata kwa kitendo cha kunyoa atawagawia watu mbalimbali.



Jessica Alba ajifungua
Staa wa filamu, Jessica Alba ametangaza kupitia mtandao wa mawasiliano wa Facebook kuwa amejifungua mtoto wa kike.
"Nina imani mashabiki wangu mnafurahia maisha," aliandika Jessica. "Mume wangu Cash na mimi tunapenda kutangaza kuwa tumepata mtoto wa kike, Haven Garner Warren. Alizaliwa wiki iliyopita. Ninapenda kuwashukuru wote kwa kuniunga mkono."

Februari, mwaka huu, Jessica alieleza kupita Facebook kuwa alikuwa mja mzito.
Nyota huyo alioana na Warren Casha mwaka 2008. Wana mtoto mwingine Honor.

Hayek: Situmii mkorogo
Nyota wa filamu, Salma Hayek ametoboa kuwa hatumiii dawa za kujichubua uso, maarufu kwa jina la mkorogo.
Hayek aliliambia jarida la Allure hapendi kutumia dawa za aina yoyote kujiremba uso wake.
ìHata siku moja sijawahi kupaka dawa za aina yoyote kwenye mwili wangu ili kuongeza rangi,î alisema Salma.

Salma anadai hapendi wanawake wanaojichubua nyuso zao kwa kutumia madawa.
Pia alisema hana mpango wa kufanya operesheni za kuboresha mwili wake.
"Ninapenda kubakia Mungu alivyoniuma," alisema Salma.

Serena amkana Drake
Nyota wa mpira wa tenisi, Serena Williams amepinga uvumi unaoenezwa kuwa ana uhusiano wa mapenzi na Rapa Drake.

Rapa huyo hivi karibuni alionekana kwenye mechi ya Serena huko Toronto, Canada.
Serena, hata hivyo, ameibuka na kukana vikali taarifa hizo.
"Oh, jamani! Huyu ni rafiki yangu tu," alisema. "Ina maana huwezi kuwa na rafiki wa kawaida wa kiume?"
Katika siku za karibuni kumekuwa kuna uvumi kuwa watu hao wawili wana uhusiano wa mapenzi.
Aanika siri za harusi ya Kim
Kourtney Kardashian ameanika siri za harusi ya mdogo wake Kim inayofungwa leo Jumamosi.
Harusi ya Kim inayosubiriwa kwa hamu na kutajwa kuwa ya kihistoria, inatazamiwa kuwa na vikolombwezo kibao.
Kim anayefunga ndoa na nyota wa mpira wa kikapu, Kris Humphries, atavaa gauni la harusi lililobuniwa na Vera Wang.
Kourtney alieleza pia kuwa wasimamizi wa kike wa harusi hiyo watavaa nguo za rangi ya kijani.
Alitoa siri hizo kupitia mtandao wa mawasiliano ya jamii wa Twitter.
Harusi hiyo inayofungwa leo Jumamosi katika mji wa Montecito, Marekani, itagharimu kiasi cha Dola milioni 10 (Sh. 916 milioni za Kenya).


Kim kushoto
Kim kulia

Monday, August 15, 2011

Angalia watoto wa kwetu walipopewa rungu

Hii ilikuwa katika pitapita zangu Tandaleeeee, nikawakuta watoto wa huko na Mzungu. Watoto wamepewa kamera wampige picha, mazingaombwe ndio yakaanzia hapo, hebu angalia mwenyewe


Tena wao wala Mzungu wao hakujua kama nami nilikuwa nikiwafuatilia na tena nawapiga picha


Kamera yetu mtaani, angalia mchezo huu


Hizi ni pande za Tandale jijini Dar es Salaam, hawa watoto walijiokotea kipeperushi na wakaanza kujisomea bila ya kujua kuwa nasi tunawafuatilia


mara mmoja wao akashtukia.../ Aaah anatupiga picha huyuu


Baada ya hapo nao wakaanza kusoma kwa pozi wakijua kuwa wanafuatiliwa, wanapigwa picha





Jamani hata hii ni ajira kwa watoto!! Angalia hawa!





Angalia mambo hayaaaaa!

Hapa nahisi walikuwa kama wanacheza Prakatatumba??!!

Jamani hii shule ipo hukooooo Kenya
Hata hii nayo, hukohuko kwa Kibaki

Angalia vipaji mtaani kwetu!


Angalia mtu kapewa kubwa huku akimiliki mpira, watoto wabaya hawa!
Nikagundua kuwa kuna akina Drogba wa Chelsea na Valencia wa Manchester Utd
Ona Valencia anavyonyanyasa wenzake!

Sekeseke golini