Tuesday, November 29, 2011

Mvua yaleta maafa Arusha


Mvua kubwa ya upepo iliyonyesha usiku wa kuamkia jana imesababisha mafuriko makubwa, maporomoko ya mawe kwenye Mto Kirurumo uliopo mpakani mwa Wilaya mbili za Karatu na Monduli, mkoani Arusha.

Kutokana na mvua hizo mtu mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya kuzolewa na maji kilomita nne ambako maiti yake iliokotwa.

Mbali na kifo na majeruhi huyo, mvua hizo pia zimewaacha mamia ya wakazi wa maeneo hayo bila makazi kutokana na nyumba kadhaa kusombwa na mafuriko hayo.



Watalii, wagonjwa wakwama

Idadi kubwa ya watalii, ambao jana walitarajia kuendelea na safari kwenda Hifadhi za Serengeti na Ngorongoro na wengine kurejea Arusha walikwama katika barabara hiyo na kubaki wamekaa kwenye magari.

Mmoja wa watalii hayo, Johnson Taylor kutoka Uingereza alisema alikuwa ametarajia kuwahi Arusha jana ili kusafiri kurejea nchini kwao, lakini amekwama.

“nimefika hapa tangu saa 12:00 asubuhi, lakini tumeshindwa kupita kutokana na barabara kuharibika…hii ni tatizo kubwa sasa tunafanya mawasiliano kuona kama tiketi za safari zitabadilishwa”alisema Taylor.



Wananchi waombwa

kuhama mabondeni


Mbunge wa jimbo la Karatu, Mchungaji Israel Natse na mkuu wa wilaya hiyo, Methew Sadoyeka walitoa wito kwa wananchi ambao wanaishi katika maeneo ya mabonde kuhama sasa kwani taarifa za utabiri wa hali ya hewa zimesema kutakuwa na mvua nyingi hadi Desemba.


JWTZ waenda kufungua barabara

Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), kutoka Makao Makuu ya Brigedi ya Mbuni wilayani Monduli, jana walifika eneo la tukio Mto wa Mbu kusaidia kazi ya kufungua barabara ya Karatu-Arusha ili kuruhusu magari kupita.


Rais Bashir amtimua balozi wa Kenya


RAIS Omar al-Bashir wa Sudan amemfukuza Balozi wa Kenya nchini humo, kufuatia Mahakama Kuu ya Kenya kutoa amri ya kukamatwa kwa rais huyo. Pia amemuagiza balozi wake aliyeko mjini Nairobi arejee nyumbani.

Rais Bashir ambaye anatafutwa na Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa (ICC) amempa saa 72 balozi huyo awe ameondoka mjini Khartoum.

Kwa mujibu wa Jaji wa Mahakama Kuu ya Kenya, Nicholas Ombija, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Usalama wa Ndani lazima watekeleze amri hiyo ya kumkamata iwapo Rais Bashir atakanyaga tena ardhi ya Kenya.



Habari zinasema, japokuwa Kenya ni mwanachama wa mahakama ya ICC, vyombo vyake vya usalama havikuweza kumkamata Rais Bashir wakati alipoitembelea Kenya mwezi Agosti, mwaka jana.

Kutokana na hatua hiyo, baada ya tawi la shirika lisilo la kiserikali, Tume ya Kimataifa ya Wanasheria, iliomba Mahakama Kuu itoe hati ya kumkamata. Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan awali ilijaribu kupuuza uamuzi wa Jaji huyo ikisema uamuzi huo ulikuwa ni maswala ya ndani ya Kenya, ambayo yasingeathiri uhusiano kati ya Sudan na Kenya.


Sunday, November 27, 2011

Congo yachafuka, wawili wauawa


Ikiwa leo wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanatarajia kumchagua rais wao vurugu kubwa zaendelea kushika kasi katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.

Kampeni hizo ambazo hazikumaliza katika muda uliokusudiwa na tume ya uchaguzi lakini kutokana na vurugu kubwa ambazo mpaka sasa zimesababisha watu wawili kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Juzi, polisi nchini humo ilipiga marufuku kampeni zote za uchaguzi katika mji mkuu Kinshasa baada ya wafuasi wa chama tawala na upinzani kushambuliana na kusababisha mauaji.

Licha ya vurugu hizo kuendelea nchini humo na kusababisha wananchi kuwa na wasiwasi zaidi hasa leo ambapo wanamchagua rais wao atakaoliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine pamoja na wabunge.


Wafuasi wa chama kikuu cha upinzani cha UDPS katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakiyakimbia mabomu ya machozi yaliyolipuliwa na polisi nchini humo karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa uliopo mjini Kinshasa.

Rais Joseph Kabila na mahasimu wake wakuu wawili Etienne Tshisekedi na Vital Kamerhe juzi walikuwa wamejitayarisha kufanya kampeni za lala salama za uchaguzi huo katika maeneo yanayokaribiana mjini Kinshasa hata hivyo kampeni hizo zilikatishwa na vurugu kubwa zilizoibuka mkutanoni hapo.

Habari zinasema, licha ya leo wananchi wanamchagua kiongozi wao lakini bado kuna wasiwasi kuhusu ugawaji karatasi za kupigia kura, kwa kuwa ndege zimeshindwa kufika baadhi ya maeneo kutokana na hali mbaya ya hewa.


Hivi tunaelekea wapi??!!

Thursday, November 3, 2011

Hapa ni Dar, hii ni shule

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akiangalia mmoja ya darasa lililojengwa mwaka 1978 katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam ambalo halitumiki kufuatia kuchakaa kwake na shule hiyo kushindwa kulikarabati.

Viungo vya binadamu vyampeleka jela miaka 10

Mkazi wa Kijiji cha Wami Dakawa, Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, Fatma Kachingo, akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukutwa na fuvu la binadamu eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa Morogoro muda mfupi kabla ya kuhukumiwa kifungo cha miaka 10 jela, kufuatia kukiri kosa.


Mwanamke aliyekutwa na viungo vya binadamu, amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela baada ya kukiri kosa hilo huku mume wake akirudishwa mahabusu baada ya kukana shtaka.

Hukumu hiyo ilitolewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, walipofikishwa washtakiwa hao ambao ni mume na mke; Fatuma Kachingo (42) na Mogela Victory (38), wakazi wa Kijiji cha Wami Dakawa, Wilaya ya Mvomero.

Hakimu Nuru Nassari alisema kitendo cha mshtakiwa kukiri kosa kinaifanya mahakama kuamini kuwa, alifanya kosa hilo kwa makusudi huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria na kwamba, adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa watu wengine wanaomiliki viungo vya binadamu kwa imani za ushirikina.

Kabla ya kutiwa hatiani, mshtakiwa huyo alijitetea ili mahakama impe adhabu ya huruma kwa madai kuwa, ana familia inayomtegemea wakiwamo wajukuu na umri wake ni mkubwa.

Hata hivyo, mahakama ilitupilia mbali utetezi huo baada ya upande wa mashtaka ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Lameck Wabi, kuomba kutoa adhabu kali kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya ukataji viungo unaofanywa kwa imani za ushirikina.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, washtakiwa hao kwa pamoja Oktoba 29, mwaka huu saa 2:00 asubuhi, walikutwa na fuvu na ngozi ya binadamu ambavyo vilihifadhiwa chumba kimojawapo kwenye nyumba wanayoishi.

Vitu vingine ni magamba ya konokono ambavyo vinadhaniwa vinatumika katika shughuli za ushirikina.


Htimaye Kabwe afanyiwa operesheni

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akila matunda baada ya kufanyiwa operesheni katika Hospitali ya Apollo nchini India, jana. Zitto amefanyiwa operesheni puani kutona na kusumbuliwa na maradhi ya kipanda uso.

Zitto ni kiongozi wa nne kupelekwa India kwa matibabu katika kipindi kisichozidi miezi mitatu, akitanguliwa na mawaziri wawili na naibu waziri mmoja. Hao ni Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe.

Aligundulika kuwa na maradhi hayo ya kipanda uso ambayo kitaalamu yanajulikana kama sinusitis tayari yakiwa sugu. Alisema Daktari Bingwa wa magonjwa hayo, Dk Kimaryo wa MNH alimweleza kwa kirefu juu ya tatizo hilo na kumshauri kuwa suluhisho lake upasuaji, huduma ambayo ilikuwa haipatikani katika hospitali hiyo ya Taifa.

Tuesday, November 1, 2011

Unafiki bado unaendelea, kuendelezwa huko Libya

Waziri Mkuu mpya wa Serikali ya Mpito nchini Libya, Abdel Rahim al-Kib (Kushoto) akipongezwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Mpito (NTC), Mahmoud Jabril ambaye aliahidi kujiuzulu pale nchi hiyo itakapokuwa imekombolewa kutoka katika utawala wa Muammar Gaddafi.

Mambo ya Watanzania hayoooo! Toka kwa Shivooo!

Miss Vodacom Tanzania 2011, Salha Israel (kushoto) akiwa katika vazi la ufukweni na wenzake katika maonesho ya mavazi hayo, nchini China juzi.