Thursday, August 23, 2012

Hatimaye makarani wa Sensa walipwa


SIKU moja baada ya makarani wa Sensa ya Watu na Makazi kugoma kula kiapo cha utii na kutunza siri, Serikali imewalipa posho zao ili kuendelea na kazi hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alisema makarani ambao hawakuwa wamelipwa posho zao, Serikali imeshawalipa na hakuna karani anayedai posho katika wilaya hiyo.
Rugimbana aliyasema hayo jana Dar es Salaam baada ya makarani zaidi ya 800 juzi kutishia kugoma kula kiapo cha utii na kutunza siri kabla ya kulipwa posho zao.
Alisema jana (juzi), kulikuwa na matatizo ya kifedha katika Manispaa ya Kinondoni na ndiyo maana kulikuwa na ucheleweshwaji wa kuwalipa makarani hao posho zao za mafunzo.

                                  


“Jana (juzi) kulikuwa na matatizo ya kifedha ambapo Manispaa ilichelewa kupata fedha kutoka hazina, lakini hadi jana asubuhi tulipata fedha hizo na kuwalipa makarani hao posho zao,” alisema Rugimbana na kuongeza:

“Makarani wote ambao jana (juzi) waligoma kula kiapo tuliwalipa fedha zao na kwamba kinachosubiriwa ni kuanza kwa kazi hiyo,” alisema.

Sunday, August 12, 2012

Bolt ashinda dhahabu ya tatu


LONDON, England
MWANARIADHA Usain Bolt ametwaa medali ya tatu ya dhahabu katika michezo ya Olimpiki baada ya kuiongoza timu yake ya Jamaica kushinda mbio za 4x100m za kupokezana vijiti.
Timu ya Jamaica katika mbio hizo za 4x100m ilitumia muda wa sekunde 36.84 huku wanariadha wake Nesta Carter, Michael Frater, Yohan Blake na Bolt wakishirikiana vizuri kupata ushindi huo.
Bolt ndiye alimaliza mbio hizo kwa upande wa Jamaica akipokea kijiti kutoka kwa Blake na kumaliza mbio hizo kwa ushindi na kuufanya umati wa watu uliokuwa uwanjani kushangilia kwa nguvu.
"Nimefurahi sana kumaliza mashindano yangu kwa ushindi mkubwa, yalikuwa ni mashindano mazuri, nina furaha pia kwa timu yangu kupata ushindi kwa sababu wenzangu walijituma kweli na tulijotoa kwa dhati,"alisema Bolt.
                          
                                    

Alipoulizwa kama anatarajia kufanya hivyo katika michezo ijayo ya Olimpiki itakayofanyika Rio de Janeiro, Bolt alisema,"itakuwa michezo migumu sana, hivi sasa Yohan Blake anakimbia vizuri sana, natumai pia kutakuwa na wanariadha wengi vijana katika michezo ijayo ya Olimpiki kwa hiyo itakuwa michezo migumu sana."
Wakati huohuo mwanariadha Mo Farah wa Uingereza ameshinda mbio za mita 10,000 katika michezo hiyo ya Olimpiki na kutwaa medali ya dhahabu.
Farah, 29, ambaye wiki iliyopita alitwaa medali ya dhahabu katika mbio za mita 5,000 alimaliza mbio za mita 10,000 na kuwashinda Dejen Gebremeskel wa Ethiopia na Thomas Longosiwa wa Kenya.

                                   


Farah ambaye mke wake ana mimba na anatarajia kujifungua watoto mapacha alisema,"siwezi kuamini kama nimeshinda, nilikuwa najisikia nimechoka, lakini nilipokimbia na kukaa mbele ya wenzangu nilisema natakiwa kupambana mpaka nishinde na kweli nilifanya hivyo."
Alisema,"medali zote mbili nilizozipata nazielekeza kwa watoto wangu wawili watakaozaliwa, nashukuru sana kupata medali katika michezo ya Olimpiki kwa sababu kupata medali mbili katika michezo ya Olimpiki siyo jambo dogo."
Uingereza ilikuwa haijawahi kutwaa medali ya dhahabu katika michezo ya riadha upande wa mbio ndefu katika michezo ya Olimpiki hivyo ushindi wa Farah ni faraja kubwa kwa Waingereza.

Anaconda auawa Bahari ya Shamu


Bahari ya shamu, MISRI
NYOKA wa ajabu (Anaconda) ambaye anadaiwa kuua zaidi ya watalii 320 na madereva 125 wa nchini Misri ameuawa juzi na wanasayansi pamoja na mabaharia wataalamu waliobobea katika fani hiyo wakishirikiana na madereva wa nchini Misri.
Mashujaa hao wa dunia ni pamoja na wanasayansi walioshiriki katika mchakato huo wa kumkimbiza nyoka huyo mpaka kuuawa ni pamoja na d. Karim Mohammed, d. Mohammed Sharif, d.  Mr Sea, d. Mahmoud students na d. Mazen Al-Rashidi
Majina ya madereva walioshiriki zoezi la kumuangamiza nyoka huyo mkubwa ni  Ahmed leader, Abdullah Karim, fisherman Knight, Wael Mohammed, Mohammed Haridi, spears Alvajuma, Mahmoud Shafik na a full-Sharif.


Mwili wa nyoka huyo umekuwa kivutio kwa watu wa nchi hiyo waliokusanyika kuuona mwili huo na sasa umekwishahamishiwa katika hifadhi ya Morgue katika kituo cha wanyama cha kimataifa kiitwacho Sharm El Sheikh.

Watu 250 wafariki dunia


AZARBAIJAN ,Iran
JUMLA ya  watu wasiopungua 250 wamefariki dunia kutokana na tetemeko la ardhi ambalo limetokea kwenye mkoa wa Azarbaijan Mashariki nchini Iran. 
Mkurugenzi wa Kamati ya Migogoro ya mkoa wa Azarbaijan Mashariki ulioko magharibi mwa Iran Khalil Saei alisema watu hao wamefariki dunia baada ya  tetemeko hilo la  ardhi kuyakumba maeneo ya Ahar, Varzaqan na Haris.
Raia wa Iran wakijaribu kuwaokoa wenzao walionasa katika nyumba iliyobomolewa na tetemeko la ardhi juzi, zaidi ya watu 250 walifariki dunia. Picha na AFP

Aliongeza kuwa zaidi ya watu wengine 2000 wamejeruhiwa katika tukio hilo. 
Alisema kwamba  zaidi ya Vijiji 60 vya mkoa wa Azarbaijan vimeharibiwa kwa baina ya asilimia 50 hadi 80 kutokana  tetemeko hilo na timu za uokoaji zinaendelea kutoa misaada kwa walioathirika licha ya njia na barabara nyingi kuharibiwa. 
Tetemeko hilo ambalo lilikuwa na  ukubwa wa 6.2 kwa kipimo cha Rishta ulitokea juzi jioni, kituo chake kikuu kikiwa katika eneo la Ahar. 
Tetemeko jingine kama hilo lilikuwa na  daraja 6 kwa kipimo cha Rishta lilitokea saa 12 na dakika 4 jioni katika eneo la Varzaqan

Uchungu wa kuibiwa

Msanii Mohamed Nice 'Mtunisi' akilia baada ya kukamata CD feki walizozikamata kwa kushirikiana na Kampuni ya Steps Entataiment jana, Dar es Salaam.