Monday, July 11, 2011

Kweli huyu ni shetani mwekundu!!


Shabiki wa Manchester United aliyejulikana kwa jina moja tu la Michael alitoa mpya.
Alikuwa akiangalia mechi kati ya Manchester United na Liverpool katika uwanja wa Old Trafford.
Karibu na alipokuwa amekaa Michael kulikuwa kuna kiti kitupu.
"Hicho kiti cha nani?" aliuliza mtu aliye karibu na Michael.
"Mke wangu ana kawaida ya kukaa hapa," alijibu Michael.
"Kwanini hayupo hapa?" mtu huyo alizidi kuuliza.
"Amefariki," alijibu Michael.
"Sasa kwanini haukumpa rafiki yako tiketi aje kuangalia mechi?" alihoji tena mtu huyo.
"Rafiki zangu wamekwenda kwenye mazishi ya mke wangu," alisema Michael.

Prince kumsimamia mtoto wa Beckham


Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William na mkewe Princess Kate watasimamia ubatizo wa mtoto wa David Beckham.
Beckham alikutana na watu hao jijini Los Angeles na kuwazawadia jezi ya timu yake ya LA Galaxy.
Alitumia nafasi hiyo kuwaomba William na Kate kusimamia ubatizo huo.
Beckham, alihudhuria dhifa kwa ajili yao iliyofanyika kwenye ubalozi mdogo wa Uingereza jijini Los Angeles.
Prince William na mkewe pia walimtakia kila la heri Victoria Beckham, ambaye ni mja mzito.
Beckham aliwaambia; "Victoria alitaka kuja lakini kwa sasa amechoka sana."
William alijibu; "Usiwe mpuuzi. Naomba umtumie Victoria salamu zetu."

Balotelli akodiwa mlinzi


Mshambuliaji wa Manchester City, Mario Balotelli ametafutiwa mlinzi na klabu yake.
Mabosi wake katika klabu ya Manchester City wamepanga kuajiri mlinzi na msaidizi maalum kwa ajili ya Balotelli.
Balotelli amekuwa kipenzi cha mashabiki tangu atue katika timu hiyo licha ya tabia zake kutotabirika.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Inter amefanya vituko vingi tangu atue Manchester City.
Alisababisha ugomvi mkubwa wakati wa mechi ya nusu fainali ya Kombe la FA dhidi ya Manchester United msimu uliopita.
Pia amewahi kulazimisha kutembelea gereza la wanawake ili kuona jinsi kulivyo.

Mke wa Ashley Cole aonywa


Mke wa beki wa Chelsea, Ashley Cole amerudi Marekani ili kuagana na mpenzi wake, Derek Hough.
Dereck, hata hivyo amemwonya Cheryl Cole kuhusiana na uamuzi wa kumrudia mumewe Ashley.
"Usimrudie huyo jamaa ni mtu muungwana sana."
Dereck, ambaye ni dansa amechukizwa na kitendo cha Cheryl kurudiana na mumewe na kumwonya kuwa anajitakia matatizo.
Amemwonya Cheryl hatakuwa tayari kurudiana naye ikiwa Ashley atamsaliti tena.
Cheryl, 28, alikwenda Los Angeles, Marekani akiwa amefuatana na Kimberley Walsh, ambaye wako naye kwenye bendi ya Girls Aloud.
Walipofika huko ndio walikutana na Dereck na kula naye chakula katika mgawaha wa West Hollywood.

Umbea tu, nani kawaambia mi mjamzito?


Benita Nzeribe amesimama mbele ya mapaparazi akanyoosha kidole tumbo lake akiwauliza; "Mmeona mimba humu?"
Msanii huyo ambaye amekuwa akiandamwa na tetesi kwamba ana ujauzito wa miezi tisa aliibuka kujibu tuhuma hizo na akasisitiza kuwa hana na mama yake amethibitisha.
"Walisema nina mimba ya miezi tisa na nimefanya pia harusi ya siri, sababu ni kwamba nimekuwa sionekani wala sipo sokoni. Ni sawa watu kukusema lakini inauma zaidi wanavyokutafsiri tofauti."

Cossy Orjiakor ajianika Facebook


Cossy Orjiakor ameweka namba zake za nyumbani na ofisini kwenye Facebook lakini ametaja wanaume wawili wa Nigeria ambao wanamsumbua na hawataki.
Msanii huyo ambaye ni kawaida yake kuvaa nguo zinazoonyesha sehemu kubwa ya matiti yake makubwa, ameandika kwenye ukurasa wake kwamba; "Tafadhali wanawake chungeni waume zenu. Kama umeolewa au ni demu wa Oyi Vitus Obunike na Oraniaka Patrick, tafadhali waambie wazee hawa waachane na mimi, waniache. Kama hamuwaridhishi kimapenzi nendeni mkapatiwa mafunzo."
"Tafadhali niacheni niishi maisha yangu na nyie endeleeni na yenu,"alisisitiza msanii huyo ambaye sasa anapiga picha za video za wimbo wake mpya wa 'you want me'

Yvonne Nelson sasa njia panda


Yvonne Nelson ameandika barua akiomba radhi lakini lakini mamlaka ya filamu nchini Ghana imemchunia msanii huyo kwa kutotoa tamko lolote hadi sasa.
Msanii huyo alifungiwa kushiriki katika filamu yoyote na mamlaka hiyo tangu Oktoba mwaka baada ya prodyuza Abdul Mumuni wa Venus Films kuripoti utovu wa nidhamu, ukatili na kukiuka mikataba alivyokuwa akifanya msanii huyo.
Mamlaka hiyo ambayo imejumuisha maprodyuza, wasambazaji, mashirikisho imeripotiwa kuwa huenda ikatoa tamko Alhamisi kwani tayari msanii huyo ameshampigia magoti Abdul na kukiri kosa pamoja na kukubali kufanya nae kazi kwa malipo nafuu ikiwa ni sehemu ya kujikosha.
Prodyuza huyo amemsamehe lakini mamlaka husika bado haijatoa tamko muhimu kuhusu kusamehewa kifungo chake cha mwaka mmoja baada ya kukitumikia miezi tisa sasa.

Mercy Johnson amchunia Mama G

Mercy
Mercy
Mercy
Mama G

Mercy Johnson amewaangukia mastaa karibu wote wa kike na kuwaalika kwenye harusi yake itakayofanyika mwezi Agosti lakini Mama G si mmoja wao.
Habari zinadai kuwa msanii huyo anataka harusi yake iweke rekodi kwa kuhudhuriwa na mastaa wengi zaidi ndani na nje ya Nigeria kabla ya kwenda kwenye fungate katika visiwa vya malta.
Ripoti zinasema kuwa msanii huyo amekuwa akijaribu kupatana mpaka na baadhi ya wasanii ambao alikuwa na tofauti nao huku Genevieve Nnaji akiombwa kuwa msimamizi wa mkuu wa ukumbi na shughuli zote za sherehe hiyo.
Rafiki wa karibu wa Mercy alidokeza kuwa msanii mkongwe Patience Ozokwor 'Mama G' mpaka sasa hajapigiwa simu kupewa mualiko wowote jambo ambalo linaibua mjadala kwamba bado wana bifu.

Wanasoka 10 waislamu safi barani Ulaya

Wakati mwingine ni vigumu kwa mashabiki wa soka kufahamu imani za wachezaji kutokana na majina yao. Na wakati mwingine ni vigumu kwa mashabiki kufahamu imani za wachezaji kutokana na uchache wa watu wa imani fulani katika bara fulani au nchi fulani.

Wachezaji wengi barani Ulaya wana imani ya dini ya Kikristo kutokana na historia za bara hilo zilivyo. Wafuatao ni wachezaji 10 maarufu zaidi ambao ni waumini wa dini ya Kiislamu. Wengi kati ya hao wanatoka nchini Ufaransa huku wakiwa na asili ya nchi za Afrika Kaskazini. Wengine wanatoka katika nchi za Afrika Magharibi.


Nicolas (Bilal) Anelka

MSHAMBULIAJI huyu wa Chelsea alibadili dini mwaka 2004 alipokwenda Falme za Kiarabu baada ya majadiliano ya muda mrefu na marafiki zake wa utotoni. Aliamua kuchukua jina la Kiislamu la Abdul-Salam Bilal. Anelka alikuwa mchezaji wa Manchester City wakati huo na alifikiria kwenda kucheza katika nchi moja ya falme za kiarabu lakini hata hivyo baadaye aliamua kwenda zake Uturuki kuchezea Fenerbache.


Franck (Bilal) Ribery

Franck Ribery ni mchezaji mwingine wa Kifaransa aliyeamua kubadili dini na kuwa Muislamu. Hii inatokana na mkewe ambaye ni Mfaransa mwenye asili ya Algeria kuwa muislamu anayeifuata dini yake kwa karibu. Ribery hivi karibuni alilipotiwa akisema “Nasali mara tano kwa siku, nafanya hivyo kwa sababu inaniwezesha kujihisi huru na kujisikia vizuri baadaye.”



Kolo (Habib) Toure

MLINZI huyu wa Manchester City alikulia nchini Ivory Coast na aliichezea Asec Mimosas kabla hajatua Arsenal. Toure ni muumini safi wa dini ya Kiislamu kama ilivyo kwa familia yake. Hivi karibuni alikaririwa akisema kwamba angependa kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wote waislamu wa Uingereza.


Frederick (Oumar) Kanoute

Mzaliwa huyu wa Ufaransa mwenye uraia wa Mali ambaye amestaafu kuichezea timu ya taifa ya Mali alianza kushika imani ya Kiislamu kikamilifu tangu akiwa na umri wa miaka 20 (sasa ana miaka 34). Aliwahi kukataa kuvaa jezi ya timu yake Sevilla iliyokuwa inatangaza mtandao wa Kamari, 888.com. badala yake Sevilla walimpa jezi ambayo haikuwa na maandishi hayo kifuani. Kanoute pia alinunua msikiti mmoja jijini Seville uliokuwa na thamani ya pauni 700,000.


Karim Benzema

Karim Benzema alizaliwa Ufaransa kwa wazazi wenye asili ya Algeria. Anasali kwa imani ya Kiislamu. Kwa sasa anachezea Real Madrid baada ya kuhamishwa kwa euro milioni 35 kutoka Olimpiki Lyon. Kwa sasa ana namba ya kudumu katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa.


Samir Nasri

Samir Nasri amekuwa moto katika klabu yake ya Arsenal kiasi kwamba Wafaransa wanamuona kama Zidane mpya. Kwa sasa anahusishwa kuondoka Emirates. Kama ilivyo kwa Zidane na Benzema, Nasri naye amezaliwa na wazazi wa Kialgeria nchini Ufaransa. Amekulia katika mazingira ya Uislamu ndani ya familia yao. Hata hivyo, mpenzi wake, Tatiana Golovan ambaye ni mcheza tenisi wa kike maarufu mwenye asili ya Urusi si Muislamu.


Yaya Toure

Yaya Toure ni mdogo wake Kolo Toure ambaye jina lake linajiochomoza namba tatu katika orodha ya wachezaji hawa. Kama ilivyo kwa kaka yake Kolo, Uislamu wa Yaya unaanzia katika familia yao nchini Ivory Coast. Hivi majuzi alielezwa kukerwa kwake na kitendo cha baadhi ya wachezaji wa Ligi Kuu England, hasa wale wa England kupenda kujirusha katika klabu za usiku bila aibu.


Hatem Ben Arfa

Hatem Ben Arfa ni kipaji kizuri cha soka kutoka Ufaransa. Staa huyu wa kimataifa wa Ufaransa anayechezea Newcastle amezaliwa na wazazi wenye asili ya Tunisia nchini Ufaransa. Familia yake yote ni Waislamu huku hicho kikiwa kitu kinachomfanya awe muumini safi wa dini ya Kiislamu.


Khalid Boulahrouz

Khalid Boulahrouz ambaye kwa sasa anachezea Stuttgart ana asili ya Morocco huku familia yake ikiwa ni waumini safi wa dini ya Kiislamu. Staa huyu wa zamani wa Chelsea ni Muislamu wa imani ya Sunni na familia yake yote ipo katika mkondo huo. Boulahrouz ana uraia wa Uholanzi kwa sababu amezaliwa nchi hiyo.


Abou Diaby

Abou Diaby, kama ilivyo kwa familia ya akina Toure ana asili ya Ivory Coast. Alizaliwa na kukulia Ufaransa na tayari ameshaichezea Ufaransa katika ngazi zote kuanzia timu za vijana mpaka sasa anachezea timu ya wakubwa huku mwaka jana akiwa miongoni mwa wachezaji wa Ufaransa waliochemsha katika fainali za Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini. Diaby anatoka katika familia ya Kiislamu na yeye mwenyewe ni muumini safi wa imani hiyo.


Wananmichezo wa Bongo igeni hii!


Mwanariadha wa Jamaica, alitoa mpya wakati aliposhinda mbio za mita 200 nchini Ufaransa, akiwa amevalia fulana yenye picha yake wiki iliyopita.
Hiki ni kitu ambacho Muhammad Ali angeweza kufanya wakati wa enzi yake akipigana ngumi za kulipwa.
Watu wamechukulia kuwa ni majivuno ya Bolt ya kutaka kuionyesha dunia kuwa yeye ni zaidi.

Sunday, July 10, 2011

Don't chezea Yanga!


Mashabiki wa Yanga wakishangilia mara baada ya kuwafunga watani wao wa jadi Simba 1-0 na kufanikiwa kutwaa Kombe la Kagame Uwanja wa Taifa jana

Sasa Wabongo tunaanza kuamini


Mtoto akiangalia kituo cha mabasi yaendayo kasi kinachojengwa katika makutano ya Barabara za Shekilango na Morogoro, jijini Dar es Salaam. Mradi huo inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwaka huu.

Wassira akiri kulala bungeni


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Mahusiano na Uratibu) Stephen Wasira, amekiri kulala bungeni wakati kikao cha bunge kikiwa kinaendelea lakini, akalilaumu our sister paper Mwananchi, for taking a photo of him in such a circumstance.

Juni 22 mwaka huu katika toleo lake namba 04013, gazeti hili lilichapisha picha ya Wasira akiwa amefumba macho na kuinamisha kichwa begani wakati anakaimu nafasi ya Waziri Mkuu bungeni.

"Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Steven Wasira, akitafakari wakati wabunge wakichangia Hotuba ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2011/1012. Kutokana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutohudhuria kikao cha bunge juzi na jana (20 na 21 Juni), Wasira ndiye aliyekuwa akikaimu nafasi ya Kiongozi wa Shughuli za Serikali bungeni," ilieleza picha hiyo.

Juzi jioni Wasira wakati akifanya majumuisho ya Matumizi ya Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu alilishambulia gazeti hili kwa kumpiga picha hiyo, akisema linaandika habari za uchochezi.

Alithibitisha madai yake hayo kwa kutumia picha hiyo aliyopigwa akionekana amelala bungeni.

“Gazeti hili lina mlengo wa kigeni kila wakati linafanya mambo ya kichochezi, hawafai hawa,” alisema Wasira.

Wasira alikiri kuwa alikuwa amesinzia wakati Bunge likiwa linaendelea lakini, akasema kitendo cha gazeti hili kutoa picha yake akionekana amelala, ni uchochezi.

“Mheshimiwa Spika, mimi siku ile nilikuwa najisikia vibaya nikapitia hapo dispensary (zahanati ya Bunge) wakanipatia dawa ya mafua,”alijitetea Wasira ambaye ni mbunge wa Bunda akibainisha kuwa kwa kawaida, dawa aliyopewa ina tabia ya kusababisha usingizi.

Kwa mujibu wa Wasira Gazeti la Mwananchi lilitoa picha hiyo kwa lengo la kuchochea huku akitaja baadhi ya habari alizodai kuwa ziliwahi pia kutolewa na gazeti hili kwa lengo la uchochezi.

“Kwa mfano gazeti hili liliandika ‘Vita ya Lowassa, Serikali ya JK sasa wazi’ na nyingine ikaandika ‘Chadema yaibwaga CCM kuhusu posho,” alisema Wasira huku akinukuu vichwa vya habari hizo.

Wasira ametoa mtazamo wake huo dhidi ya gazeti hili, karibu wiki mbili tangu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Augustino Mrema kulisifu Mwananchi kuwa ni gazeti Makini, linalotoa habari za kweli na uhakika. Mrema pia aliwahi kupigwa picha na gazeti hili akiwa amelala bungeni.

Vile vile mashambulizi ya Wasira yamekuja wakati wabunge kadhaa wamekuwa wakitumia habari zilizoandikwa na gazeti hili nukuu habari za gazeti hili kujenga hoja zao bungeni, wakilieleza bunge kuwa kutokana na umakini wake, habari zinazoandikwa na Mwananchi ni za kuaminika.

Mmoja wa wabunge hao ni Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Susan Lyimo ambaye akitumia nukuu za gazeti hili aliliambia bunge kuwa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (PTF) umekuwa ukijihusisha na vitendo vya kitapeli.

“Mfuko huu umekuwa na tuhuma za kuwatapeli wananchi kwa kuwapa ahadi za wongo au zisizotimizwa kwa wakati. Mathalani Julai 15 mwaka jana, zaidi ya wanachama 200 wa mfuko huo wa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam walivamia ofisi ya makao makuu ya taasisi hyo yaliyopo Morocco Jijini Dar es Salaam wakilalamika kutapeliwa fedha zao za amana,” alilalamika.

Susan akionyesha kuwa taarifa hizo ni kwa mujibu wa Gazeti la Mwananchi la Julai 2010 pamoja na mtandao wa YouTube, alifafanua kuwa wanachama hao walikuwa wameambiwa watoe Sh18,000 kama kiingilio cha uanachama na amana ya Sh250,000 kwa ahadi ya kukopeshwa Sh1 milioni ndani ya kipindi cha wiki moja.

Mbaya zaidi alisema, wanachama hao waliongezewa vifungu vya masharti kwenye mikataba hiyo tofauti na awali hivyo kuwaweka katika wakati mgumu wa kupata mikopo waliyokusudia.

“Mheshimiwa Spika, wananchi wamefikia hatua ya kuufananisha mfuko huu wa rais na kampuni ya DEC ambayo ambayo inatuhumiwa kuendesha mchezo wa upatu kinyume cha sheria,” alisema Susan katika hutuba hiyo ya Kambi ya Upinzani wakati ambapo pia bajeti ya Mahusiano na Uratibu Ofisi ya Rais, ilikuwa imesomwa na Wasira.

Alisema PTF ilianzishwa kwa lengo l kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini kwa kuwapamikopo na maarifa lakini malalamiko ya wananchi yanaashiria mfuko huo unaenda kinyume na kazi hiyo.

“Tumegundua kuwa mikopo inayotolewa na mfuko huu imekuwa na riba sawa na taasisi nyingine zinazofanya biashara ya kukopesha fedha,” alilalamika akifafanua:

“Sisi kambi ya upinzani tunahoji, je faida inayotengenezwa na mfuko huu inakwenda wapi? Mbona haionekani kwenye mapato ya serikali?”

Kibaya zaidi kwa PTF aliema

Kwa sababu hiyo, Susan alilitaka Bunge kujadili mwenendo na utendaji wa mfuk huo na kushauri njia bora ambayo itakuwa kwa maslahi yaliyokusudiwa.

Hamza anateseka, waliosababisha wanakula raha




Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), imethibitisha kuwa maisha ya Juma Hamza (12), aliyejeruhiwa kwa risasi na polisi wa Kituo cha Chang’ombe, Wilaya ya Temeke, yapo mashakani kutokana na majeraha aliyopata kwa kupigwa risasi sehemu ya tumbo.

“Ini liliraluliwa, kifuko cha kutunzia uchafu unaotoka kwenye ini kilitobokatoboka, utumbo umetanuka na kuna tundu ndani ya kibofu chake cha mkojo,” maelezo ya kidaktari yaliyo kwenye hati ya polisi ya matibabu (PF3) yanaeleza.

Mwezeshaji wa haki jamii Mtaa wa Mgurumbasi A, Kata ya Keko, Issa Ndambwi, anayeshughulikia masuala mbalimbali ya mtoto huyo alilieleza Mwananchi kuwa, mama yake Hamza alipompeleka kliniki wiki iliyopita, alishauriwa na daktari kuwa ikiwa wanakusudia kuchukua hatua za kisheria, wafanye hivyo mapema iwezekanavyo.

Ndambwi alisema hivi sasa kinachohitajika ni msaada wa kisheria ili kesi dhidi ya waliosababisha madhara kwa mtoto huyo ifunguliwe na kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma ili ikithibitika, haki stahiki kwa mtoto zitendeke.

Alisema wazazi wa Hamza hawana uwezo wa kumudu gharama za kuendesha kesi, hivyo anaomba yeyote mwenye uwezo na moyo wa kumsaidia mtoto huyu, kitaalamu (kisheria) au kwa fedha awasiliane na uongozi wa gazeti hili kufanikisha dhamira ya kufungua kesi haraka kama ambavyo imeshauriwa na daktari anayemtibia.

Polisi mmoja wa Kituo cha Chang’ombe anatuhumiwa kumjeruhi tumboni kwa risasi mtoto huyo usiku wa kuamkia Oktoba 24, mwaka jana. Jeshi hilo lilieleza kuwa, Hamza alijeruhiwa kwa bahati mbaya wakati askari wakikamata watuhumiwa wa unyang’anyi kwenye ukumbi wa Jumba la Dhahabu, Keko Molemo.

Hata hivyo, wakazi wa eneo la Magurumbasi A anakoishi Hamza, walipinga vikali taarifa hiyo wakisema hakuna ukumbi wenye jina hilo eneo lilipotokea tukio hilo na kwamba, waliokamatwa ni baba mzazi wa Hamza na mpangaji mwenzake, waliotolewa vyumbani mwao walimokuwa wamelala na familia zao.

Hamza alifanyiwa upasuaji mkubwa wa pili, Mei 4, 2011 na kuruhusiwa Mei 15, akitakiwa kurejeshwa hospitalini siku tatu baadaye ili atolewe nyuzi kwenye kidonda. Lakini, uongozi wa wodi aliyokuwa amelazwa ulimnyima hati ya ruhusa kwa sababu alikuwa akidaiwa Sh50,000, hadi Juni 2, mwaka huu deni lake lilipolipwa.

Malipo hayo yalipofanywa na hati za ruhusa kukabidhiwa kwa familia ya mtoto huyo, ilibainika kuwa alitakiwa kutumia aina nne za dawa ambazo mpaka wakati huo hakuwa amezitumia na kidonda kuanza kuoza kwa kutoa maji yaliyochanganyika na usaa. Taarifa ya daktari inayoeleza kuwa mtoto huyo ameharibika vibaya katika maungo yake ya ndani, inakuja huku kukiwa na malalamiko kwamba hali hiyo inachochewa na huduma zisizoridhisha ambazo amekuwa akipata mtoto huyo.

Hii kalii!


Askari magereza wanaume mkoani Morogoro kutoka katika magereza za Kingolwira,Mtego wa simba, mahabusu mkoa, Kihonda, ofisi kuu ya gereza mkoa, Mkono wa mara, Chuo cha gereza KPF na Gereza la Kingolwira wakishindana kukuna nazi katika tamasha la askari magereza lililofanyika Kingolwira manispaa ya Morogoro.

Brazil, Argentina zajiwekea mazingira magumu Copa America


Mshambuliaji wa Brazil, Neymar (kulia) akijaribu kumtoka beki wa Paraguay, Dario Veron (katikati) na kiungo Enrique Vera wakati wa mechi ya Kundi B ya michuano ya Copa Amerika iliyofanyika kwenye Uwanja wa Mario Kempes mjini Cordoba, umbali wa Km 770 Kaskazini Magharibi mwa Buenos Aires. Mechi hiyo ilimalizika kwa sare 2-2.

Wazazi wa Ashley Cole na Chery watofautiana!


Kufuatia kurudiana kwa Ashley na Chery, wazazi wao wameonyesha hisia tofauti juu ya kurudiana kwao. Wakati mama yake Ashley,akionyesha kufarijika na kitendo hicho, mama wa wa Chery, Joan Callaghan ameonekana kukerwa na kitendo hicho kiasi cha kutoa maneno makali kwa mwanawe.
"Sitaki kabisa arudiane nayeî, aliongea mama huyo katika sherehe ya kuzaliwa kwa mwanawe huyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. "Siwezikumsamehe kwa kile alichomfanyia mwanangu" alisisitiza.

Jolie alipwa kuliko yeyote Hollywood!


Si kwa sababu ya kuchangia sana kwenye maonesho ya hisani na wala si kwa ajili ya mauzo makubwa yaliyosababishwa na filamu ya Salt lakini ukweli ni kwamba, kiwango kimepanda na binti anashikilia kileleni kwa kuwa muigizaji kutoka Hollywood ambaye analipwa zaidi kuliko wote kwa sasa, kwa upande wa mabinti.
Huyu na mwenzake Sarah jessicah parker ndio wanawake ambao kwaq mwaka mmpoja na nusu sasa wamebakia kwenye kiwango cha kulipwa dola za kimarekani 30,000 iwapo utataka waingie kwenye filamu yako, fedha ambayo kwa sasa imevunja rekodi huko Hollywood.

Nyota Ndogo anavyoyakabili maisha


Nyota ndogo amesema hatua za maisha alizozipitia hadhani kama ilikuwa kwa bahati mbaya. "Ni hali ya kawaida kwa sisi binadamu na nadhani Mungu ana makusudi yake kukupitisha binadamu katika hatua azitakazo yeye, kwani sikuwahi kudhani wala kufikiria kama ningekuwa hapa nilipo.
"Awali nilikuwa nikisoma katika moja ya shule za Sekondari mjini Mombasa lakini hali ya maisha ilikuwa ngumu kiasi kwamba nikalazimika kuacha shule na kutafuta kazi za ndani ambazo nilizifanya kwa kipindi cha miaka kadhaa" anasema msanii huyo ambaye wikiendi iliyopita alitumbuiza katika tamasha la Serengeti Fiesta 2011 mjini Dodoma, Tanzania.

Tuesday, June 21, 2011