Monday, October 24, 2011

Gaddafi mafanikio, wosia wake waanikwa



SIKU chache baada ya kuuawa kwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, walibya na dunia kwa ujumla imeingia katika mitizamo tofauti kuhusu kiongozi huyo huku wengi wakikumbuka mafanikio aliyoleta kwa taifa hilo tofauti na viongozi wengine waliong’olewa kwa udikteta.

Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikimtangaza na kutafuta namna zote za kujenga picha ya udikteta bila kuangalia upande wa pili wa Libya iliyooachwa na Gaddafi.

Baadhi ya mambo ambayo yamekuwa yakizungumziwa ni iwapo Libya ya sasa itaweza kuneemeka na kile ambacho ilikuwa ikipata kutoka kwa kiongozi huyo, ambaye hivi karibuni aliuawa na wapinzani wake.

Gaddafi, tofauti na viongozi wengine waliowahi kutajwa kuwa madikteta duniani, ana mengi ya kukumbukwa na kusifiwa kwayo.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kiuongozi wamekuwa wakieleza kusikitishwa kwao na kutotambua aina ya demokrasia ambayo baadhi ya watu wa Libya wanaililia kwa sasa na iwapo itaboresha au kuharibu kabisa maisha yao.

Hii inawekwa wazi kwamba pamoja na kwamba Gaddafi ametumia fedha nyingi za Libya katika masuala binafsi, lakini je, kwa wastani Libya ni maskini? Wapo viongozi waliozitumia nchi zao na kuziharibu kabisa, Gaddafi aliwahi kuifilisi Libya?


Haya ni baadhi ya mambo ambayo Gaddafi aliyasimamia na kuyatekeleza katika utawala wake wa miaka 42 kwa Libya.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na tovuti za mawasiliano za Libya na Zimbabwe zimeeleza kuwa nchini Libya hakuna mwananchi aliyewahi kulipa bili ya umeme, umeme ulikuwa bure kwa raia wake wote.

Hakukuwa na riba katika mikopo, benki zote Libya zilikuwa chini ya Serikali, mikopo ilitolewa kwa wananchi bila riba ya kiasi chochote .

Taarifa hizo zikafafanua kuwa makazi ni haki ya msingi nchini Libya, Gaddafi aliwahi kusisitiza kwamba wazazi wake hawawezi kupata makazi hadi kila raia apate makazi. Baba wa Gaddafi alifariki dunia wakati yeye, mama yake wakiwa wanaishi katika hema.

Wanandoa wote wapya nchini humo walipata Dola 50,000 kwa Serikali kwa ajili ya kununua makazi yao kuwasaidia kuanzisha familia mpya.

Elimu na huduma za kiafya vilitolewa bure. Wakati Gaddafi nachukua nchi asilimia ya waliokuwa na elimu ilikuwa 25, kwa sasa inafikia 83.

Kwa waliotaka kuwa wakulima, walipewa ardhi bure, nyumba katika shamba lao, vifaa, mbegu na mifugo kwa ajili ya kuanzisha miradi .

Iwapo kuna waliokuwa hawawezi kupata huduma za elimu na afya wanazostahili, Serikali iliwalipia kwa ajili ya kuzipata nje ya nchi, hizi hazikuwa bure, walitakiwa kuchangia, walipata Dola2,300 kwa mwezi kwa ajili ya makazi na usafiri.

Kwa waliokuwa wakitaka kununua magari, Serikali ililipia kwa asilimia 50 ya bei. Bei ya petroli ilikuwa karibu na bure, lita ililipiwa kwa Dola 0.4.

Libya haidaiwi nje, pia ina akiba inayofikia Dola150 bilioni nje ambayo kwa sasa imezuiliwa.

Kwa waliomaliza vyuo, Serikali iliwapatia posho sawa na mshahara wa maofisa hadi watakapopata ajira yenye uhakika. Sehemu ya mauzo ya mafuta ya Libya iliwekwa moja kwa moja kwenye akaunti ya raia wake.

Kila mwanamke aliyejifungua alipata posho ya Dola5000, mikate 40 iliuzwa kwa dola0.15, asilimia 25 wa Walibya, wana shahada ya chuo kikuu.

Kama hiyo haitoshi taarifa hizo zimeeleza kuwa alisimamia mradi mkubwa kabisa wa umwagiliaji, uliopewa jina la Great Man-made River, kuhakikisha maji yanakuwepo kwenye maeneo yote ya nchi yenye jangwa.

Wakati wa vikwazo kwa Serikali yake miaka ya 1980, Libya ilikuwa miongoni mwa nchi tajiri kabisa kwa msingi wa pato la ndani, ikwa na kiwango cha juu cha maisha kuliko Japan. Ilikuwa ni nchi tajiri kuliko zote kabla ya vuguvugu la mapinduzi.

Wastani wa kiwango cha maisha kwa pato la kichwa ni Dola11,314 . Gaddafi amewahi kutumia fedha nyingi kwa ajili ya safari zake na miradi yake, lakini amefanya mabo makubwa ambayo hakuna dikteta aliyewahi kuyafanya kwa watu wake. Alirejesha pato kwa watu wake, aliwajali.

Wosia wa Gaddafi kabla ya kifo

Katika wosia wake, Kanali Gaddafi aliwaasa wafuasi wanaomuunga mkono kuendelea kupambana.

Alielezea msimamo wake kuwa amechagua kupambana hadi hatua ya mwisho na kufia katika ardhi ya Libya kuliko kuchagua njia nyepesi, ambayo kwa mtizamo wake, ni kitendo cha kujidhalilisha kisichokuwa na heshima, kukimbilia uhamishoni nje ya nchi yake, ambapo tayari alishapata ahadi nyingi za ulinzi.

Katika lugha ya Kiingereza, waraka wake wa wosia umetafsiriwa ukisomeka: “Hii ni hiyari yangu. Mimi Muammar bin Mohammad bin Abdussalam bin Humayd bin Abu Manyar bin Humayd bin Nayil al Fuhsi Gaddafi, ninaapa kwamba hakuna Mungu mwingine zaidi ya Allah na Muhammad ni Mtume wake, amani iko kwake. Ninaahidi nitakufa nikiwa Muislamu.

“Iwapo nitauawa, nitapenda kuzikwa kwa mujibu wa taratibu za kiislamu, nikiwa nimevaa mavazi nitakayokuwa nimevaa wakati kifo change kikitokea, bila mwili wangu kuoshwa, katika makaburi ya Sirte, jirani na familia na jamaa zangu.



“Nitapenda kwamba familia yangu, hasa wanawake na watoto, watunzwe vyema baada ya kifo changu. Watu wa Libya wana wajibu wa kulinda wasifu, mafanikio, historia na heshima ya waasisi na mashujaa wake.

“Watu wa Libya hawatakiwi kupuuza kujitapa na lazima wawe watu huru wa kuthaminiwa. Ninawataka wale wanaoniunga mkono kuendelea kupambana, kuwakabili wote wanaosimama kutoka nje dhidi ya Libya, leo, kesho na siku zote.

“Hata kama hatutashinda mapema, tutatoa funzo kwa vizazi vyetu vijavyo, kwamba kuchagua kulinda utaifa ni heshima na kuliuza ni uasi mkubwa ambao historia haitausahau milele, pamoja na juhudi za wengine kuwaeleza kinyume cha hayo”.

Kifo cha Gadafi Gaddafi na udhalilishaji wa maiti yake, mwanaye!


KUNA mvutano kuhusu mazishi ya marehemu Kanali Muammar Gaddafi, watu wa kabila la kiongozi huyo wa zamani wa Libya, wanadai mwili wa ndugu yao ili wauzike kwa heshima, wakati Baraza la Mpito linaweka ngumu na kusisitiza kwamba atazikwa kwa siri kubwa.

Ijumaa Wikienda, limenasa maisha ya Gaddafi saa 18 kabla ya kifo chake pamoja na danadana za mwili wa kiongozi huyo ambaye neno lake, harakati zake na fedha alizomwaga katika ufadhili, ndivyo viliwezesha kuundwa kwa Umoja wa Afrika.

Jumamosi iliyopita, Mwenyekiti wa Baraza la Mpito (NTC), Mustafa Mohammed Abdul Jalil alitarajiwa kwenda jijini Misrata kutoa tamko kuhusu mazishi hayo.

Kwa mujibu wa mtu anayedaiwa alikuwa mlinzi wa Gaddafi kabla ya kumgeuka dakika za mwisho, saa 18 kabla kiongozi huyo wa zamani wa Libya kufariki dunia, alizitumia kusali na kuweka mikakati ya kuhama Jiji la Sirte.


Wakazi wa Libya wakishuhudia mwili wa mtoto wa Gaddafi huku wakiufungua kinywa chake na kuupiga picha


Jumamosi iliyopita, Mwenyekiti wa Baraza la Mpito (NTC), Mustafa Mohammed Abdul Jalil alitarajiwa kwenda jijini Misrata kutoa tamko kuhusu mazishi hayo.

Kwa mujibu wa mtu anayedaiwa alikuwa mlinzi wa Gaddafi kabla ya kumgeuka dakika za mwisho, saa 18 kabla kiongozi huyo wa zamani wa Libya kufariki dunia, alizitumia kusali na kuweka mikakati ya kuhama Jiji la Sirte.

Mwanahabari wa Daily Mail, Andrew Malone, akishuhudia mwili wa Kanali Muammar Gaddafi.

Aliongeza kusema: “Aliwaambia wapigaji kwamba wakipata nafasi warudi kuitetea Libya na wasikubali vibaraka wa Marekani na Uingereza wafilisi mali za Walibya.”

Alisema kuwa saa tatu kabla Gaddafi na timu yake, hawajaanza kutoroka, alizungumza na wanaye kwa muda mrefu lakini akawasisitiza: “Msiumie wala msifedheheke, wakati mwingine Shetani hutumia nguvu na kufunika haki dhidi ya batili.”


Wakazi wa Libya wakishuhudia mwili wa Kanali Gaddafi na kuupiga picha


NENO LA MWISHO

Mlinzi huyo alisema, Gaddafi alijitetea kwa maneno mengi ili asiuawe lakini kauli maarufu aliitoa kwa njia ya kuuliza, “je, ninyi wanangu, mnaifahamu haki kwenye uongo?”


SAFARI YA KIFO

Alhamisi iliyopita (Oktoba 20, 2011), Gaddafi na timu yake, wakiwa kwenye magari ya kifahari, walikuwa wanahama kutoka Jiji la Sirte kuelekea mpakani. Inadaiwa walitaka kutorokea nje ya nchi, ingawa taarifa nyingine zinadai kiongozi huyo aligoma kuondoka na kusisitiza anangoja kufa kwenye ardhi aliyozaliwa.

Saa 2:30 asubuhi (saa za Libya), vikosi vya Nato na Ufaransa viliyashambulia kwa mabomu magari ya msafara wa Gaddafi. Magari 15 yaliharibiwa kwenye mashambulizi hayo, Gaddafi na timu yake walikwenda kujificha kwenye daraja la mtaro.

5:05 asubuhi, NTC ilitangaza kuwa ngome ya Gaddafi imekwisha na kilichobaki ni kutafuta masalia.

8:00 mchana, baada ya mapambano ya risasi kwisha, Gaddafi aligundulika yupo kwenye daraja la mtaro wa maji machafu amejificha.


Mwanahabari wa Daily Mail, Andrew Malone, akishuhudia mwili wa Kanali Muammar Gaddafi.


8:45 mchana mwanaume mmoja mkazi wa Sirte aliliambia Shirika la Utangazaji la Reuters kuwa alimuona Gaddafi akipigwa risasi tumboni kwa bastola yenye ukumwa wa 9mm.

8:56 mchana, Reuters ilitangaza kuwa Gaddafi alifariki dunia kutokana na majeraha baada ya mapigano ya risasi.

9:00 mchana, wapiganaji wa NTC walianza kuzunguka mitaani wanashangilia kukamatwa na kuuawa kwa Gaddafi.


10:31 alasiri, AFP ilitangaza kuwa mtoto wa Gaddafi, Muttasim amekutwa ameuawa jijini Sirte.

11:52 jioni, mwili wa Gaddafi ulifikishwa Misrata.

1:50 jioni, Aljazeera ilitangaza kuwa mtoto wa Gaddafi, Saif al Islam naye ameuawa kwenye mashambulizi hayo. Ingawa taarifa za baadaye zinasema kuwa Saif mikono yake ilikatika katika mashambulizi.

Wakazi wa Libya wakishuhudia mwili wa Kanali Gaddafi na kuupiga picha.
MAMIA ya wakazi wa Libya jana walikusanyika kushuhudia mwili wa Muammar Gaddafi mjini Misrata. Mwili wa Gaddafi ulikuwa umehifadhiwa katika chumba kimoja kilichopo eneo la biashara mjini Misrata, ambapo ulipelekwa siku ya Alhamisi alipouawa.

Maajabu ya Muammar Abu Minyar al-Gaddafi


1. There is *no electricity bill* in Libya; electricity is free for all its citizens.

2. There is *no interest on loans*, banks in Libya are state-owned and loans given to all its citizens at 0% interest by law.

3. *Home* considered a human right in Libya – Gaddafi vowed that his parents would not get a house until everyone in Libya had a home. Gaddafi’s father has died while him, his wife and his mother are still living in a tent.

4. All newlyweds in Libya receive *$60,000 Dinar* (US$50,000) by the government to buy their first apartment so to help start up the family.

5. Education and medical treatments are free in Libya. Before Gaddafi only 25% of Libyans are literate. Today the figure is 83%.

6. Should Libyans want to take up *farming* career, they would receive farming land, a farming house, equipments, seeds and livestock to kick-start their farms – all for free.

7. If Libyans cannot find the education or medical facilities they need in Libya, the government funds them to *go abroad* for it – not only free but they get US$2,300/mth accommodation and car allowance.

8. In Libyan, if a Libyan buys a *car*, the government subsidized 50% of the price.

9. The price of *petrol* in Libya is $0.14 per liter.

10. Libya has *no external debt* and its reserves amount to $150 billion – now frozen globally.

11. If a Libyan is unable to get *employment* after graduation the state would pay the average salary of the profession as if he or she is employed until employment is found.

12. A portion of Libyan *oil sale* is, credited directly to the bank accounts of all Libyan citizens.

13. A mother who *gave birth* to a child receive US$5,000

14. 40 loaves of *bread* in Libya costs $ 0.15

15. 25% of Libyans have a *university degree*

16. Gaddafi carried out the world’s largest *irrigation* project, known as the Great Man-Made River project, to make water readily available throughout the desert country.


Which other dictator has done much good to his people besides.


*P.S. If this is the dictator Gaddafi is, then give us one like him here in Bolehland


Wasifu wa Kanali Muammar Gaddafi





Alikuwa mtoto wa wafugaji wa Kibedui, mwenye maisha ya utata, lakini ambaye alitukuzwa sana, huku mataifa ya Magharibi yakimuona mtu wa hatari wakati wote.

Muammar Muhammad Gaddafi aliitawala Libya kwa zaidi ya miaka 40. Hadi mwanzoni mwa Machi 2011, alikuwa akiamini ndani ya moyo wake kwamba watu wake walikuwa wakimpenda na kwamba walikuwa tayari kumlinda hadi kufa kwa ajili yake.



Lakini wakati huo, tayari Gaddafi alikuwa ameshatumia njia za kikatili kuyazima maandamano dhidi yake, maandamano ambayo baadaye yaligeuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kwa mujibu wa taarifa, watu zaidi ya 30,000 waliuawa kwenye vita hivyo. Mara nyingi sana, Gaddafi alitoa matamko makali wakati wa vita hivyo, ila linalojuilikana zaidi ni lile la kuwaita wapinzani wake kuwa ni panya.

Kwa kila hali, yaliyotokea ni mambo ambayo Gaddafi hakuyatarajia asilani. Mtoto huyu wa wafugaji wa Kibedui aliyezaliwa mwaka 1942, alikuja kuibuka kama mkombozi wa Walibya, alipompindua Mfalme Idriss hapo mwaka 1969.

Kuanzia hapo akaanza kujenga kile alichokiona mwenyewe kuwa ni mfumo wa kidemokrasia wa moja kwa moja. Alianzisha kamati za umma zilizoamua juu ya mustakabali wa umma na wa Serikali. Aliuita mfumo wake wa kisiasa na kiuchumi kuwa ni wa kisoshalisti, alioufafanua kwenye kijitabu chake cha Kijani.


Historia yake kiufupi

Alizaliwa mwaka 1942 katika eneo la Jangwa, kwenye mji wa Sirte, katika familia ya baba Mohamed Abdulsalama Abuminiar na mama Aisha Ben Niran. Alijiunga na Jeshi la Libya mwaka 1965.

Alifanya mapinduzi ya Serikali yasiyo ya umwagaji damu na kumuondoa mfalme Idris katika utawala wake mwaka 1969 na kuwa mtawala wa Libya akiwa na umri wa miaka 27.

Alikuwa maarufu kwa nguo anazopenda kuvaa na walinzi wa kike wenye kubeba silaha, kiongozi huyo wa Libya pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.

Baada ya miongo miwili ya kutengwa katika jamii ya kimataifa, mwaka 2003, Tripoli ilikiri kuwa walifanya shambulio la Lockerbie kwa kuiangamiza kwa mabomu ndege ya Pam Am. Umoja wa Mataifa (UN) ulikubali kuondoa vikwazo dhidi ya Libya.

Baada ya miezi kadhaa, Serikali ya Kanali Gaddafi ilisitisha mipango yake ya kuunda silaha za maangamizi na hii ikarejesha ushirikiano na nchi za Magharibi.




Gaddafi ni mtu wa kipekee katika kauli zake, mienendo yake, tabia zake na mikakati yake, kwa mujibu wa Saas Djebbar, mtaalam wa siasa za Libya.

Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.

Alipanga njama ya kupindua utawala wa kifalme alipokuwa mwanafunzi wa kijeshi alipokuwa mafunzoni Uingereza kabla ya kurejea nyumbani Libya. Alipanga mapinduzi ya Septemba 1, 1969 akiwa katika mji wa Benghazi.

Alianza kujenga itikadi zake za kisiasa mwaka 1970 na kuziandika katika kitabu chake cha kijani kibichi.

Alikitumia kitabu chake kuanzisha mfumo wa kisiasa uliojumuisha kanuni za Kiislamu na mfumo ulio tofauti na siasa za ujamaa au ubepari.

Mwaka1977 aliasisi mfumo ujulikanao kama 'Jamahiriya' au 'Taifa la Umma' ambapo raia ndio wanaoendesha uongozi wa nchi yao kupitia 'kamati za umma'.

Mfumo huo wa Gaddafi umevuka mipaka na hauhusishi mambo ya siasa tu, bali pia mambo mengine.

Akiwa safarini ng'ambo, alikuwa akitumia makazi maalum kwenye kambi iliyojengwa na hema yake ya kifahari ya Kibeduwi akiwa amefuatana na walinzi wanawake ambao, inasemekana, huwa hawapotezi umakini kazini kama walinzi wanaume.


Hema hiyo pia ilitumiwa kuwalaki wageni wa Libya na Kanali Gaddafi huendesha mikutano na mahojiano yake humo humo akipepea usinga au tawi la mitende.

Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alimwita Gaddafi 'mad dog' yaani 'mbwa kichaa' na Marekani ililipiza kisasi dhidi ya Libya kwa madai ya kuhusika na mashambulio ya anga barani Ulaya kwa kuvamia miji ya Tripoli na Benghazi mwaka 1986.

Aliposhindwa katika jitihada zake za kuzipatanisha nchi za Uarabuni katika miaka ya 90, Kanali Gaddafi alielekeza nguvu zake barani Afrika na kupendekeza 'Muungano wa Nchi' za bara la Afrika.

Alianza kuvaa mavazi yake binafsi, sare za michezo zilizo na ngao za Bara la Afrika au picha za viongozi kutoka bara hilo.

Aliwahi kuvunja na kufuta Wizara za nchi hiyo pamoja na bajeti zao, isipokuwa Wizara chache ikiwemo ya Ulinzi, Fedha na Mambo ya Nje.



Licha ya uchumi wa Libya kutoa fursa kwa wawekezaji wa nje, mabadiliko bado yanakwenda taratibu.

Vuguvugu la mageuzi dhidi yake lilipoanza mwanzoni mwa mwaka huu, aliapa kuwafuata wanaompinga nyumba hadi nyumba, mlango kwa mlango, hatua iliyoibua hasira na kuchochea harakati za kijeshi dhidi yake.

Baada ya baadhi ya askari kutangaza kujitoa katika jeshi lake na kuanzisha uasi, aliapa kwamba atapambana hadi tone la mwisho la damu litakapomwagika. Alisisitiza kwamba kamwe hatakimbia kutoka katika ardhi ya Libya, atafia katika ardhi ya mababu zake.

Thursday, October 20, 2011

Gadhafi, Libya's leader for 42 years, killed


Waasi wa Libya wakiangalia tundu linalodaiwa alijificha aliyekuwa kiongozi wa Nchi hiyo Muammar Gaddafi kabla ya kukamatwa


Raia wa Libya wakisherehekea mjini Tripoli baada yakusikia aliyekuwa kiongozi wa Nchi hiyo Muammar Gaddafi amekamatwa na waasi


Hapa ni mwili wake baada ya kuuawa


Early Thursday morning, reports started emerging out of Libya that former strongman Moammar Gadhafi had been killed in a NATO-led airstrike. Later in the day, opposition National Transitional Council leader and interim government prime minister Mustafa Abdel-Jalil confirmed reports of Gadhafi's death, according to the Associated Press. NATO and the White House have yet to independently confirm the reports.


The NTC information minister told Reuters, "He was killed in an attack by the fighters. There is footage of that." If the news is confirmed, the episode would make Gadhafi the first leader killed as a result of the Arab Spring uprisings, the Associated Press notes in its obituary of the leader, which it published at 10:53 EST.

According to reports from multiple sources, Gadhafi was fleeing a NATO-led rebel attack on the former leader's hometown of Sirte, which had been a last remaining stronghold for Gadhafi forces. According to the Reuters' report, the rebels found the former Libyan strongman hiding in a hole in the ground; the rebel fighter who found Gadhafi said that the Libyan leader repeated "Don't shoot, don't shoot" upon his capture. The BBC reported that the same rebel fighter was "brandishing" a golden pistol which he said belonged to the Libyan strongman.

Thursday, October 6, 2011

Kazi ni kazi, Wanaume wakishesha

Wavuvi wakiwa kazini katika kina kirefu cha bahari ya Hindi kati ya Dar es Salaam na Mji wa Bagamoyo juzi. Wavuvi wengi bado wanatumia zana duni hali ambayo inahatarisha usalama wao.

Kikosi cha Gaddafi chatoa ‘kichapo’ kwa waasi


WAKATI watawala wapya wakiamini kwamba aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi analindwa na wakazi wa Jangwani karibu na mpaka wa Libya na Algeria, waasi 11 wameuawa Bani Walid.

Idadi hiyo ya watu ambayo ni miongoni mwa vikosi vinavyompinga Muammar Gaddafi wameuawa kwa makombora katika mapambano makali yanayoendelea nchini Libya katika mji wa Bani Walid.

Baraza la Taifa la Mpito nchini humo NTC lilikiri kuuawa kwa wapiganaji wake 11 katika mapambano hayo makali na vikosi tiifu kwa Gaddafi.


Waasi wa Libya wakiwa mile 3 kuufikia ,mji wa alikozaliwa aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi wa Sirte,jana wakiwa wanavurumisha wa kwanza kushoto akionekana akizuba masikio kutokana na milio wa mabomu hayo

Hasara kubwa zaidi imepatikana katika mji wa Sirte ambapo wapiganaji wa Baraza hilo la Taifa la Mpito wanapambana kuingia katikati ya mji huo mkubwa ulioko katika bahari ya Mediterranean na mahala ambapo kuna nyumba ya Gaddafi na mahandaki ya kijeshiMapigano hayo ambayo yaliendelea hadi usiku juzi yalijikita karibu na hoteli ya Mahari, mashariki ya Sirte, wapiganaji waasi walipigana na vikosi tiifu kwa Gaddafi na kupoteza wapiganaji 10.Hayo yameelezwa na kamanda mmoja wa Baraza la Taifa la Mpito kwa sharti la kutotajwa jina kutokana na unyeti wa habari hizo.

Kwa mujibu wa kamanda huyo wapiganaji wao na wale vichwa ngumu wa Gaddafi wamekuwa kwenye mapambano ya barabarani na kushambuliana kwa kutumia bunduki za Kalashnikovs na maguruneti yanayovurumishwa na roketi.


Steve Jobs Earned His Place in the American Business Pantheon


Steve Jobs, who died on Wednesday, was a singular figure in American business history. He will go in the pantheon of great American entrepreneurs, inventors, and innovators, alongside John D. Rockefeller, Henry Ford, and Sam Walton.

Jobs didn't invent computer technology, or the cell phone, or the notion of digitizing music. But he invented methods, business models, and devices that turned each into significantly larger cultural and economic phenomena.


To a degree, one might look back on the arc of Jobs's career and conclude that he simply rode a series of technological waves. But Jobs, and the company he led, rode the waves while pushing back against them.

In an industry frequently hostile to design, Jobs's Apple banked on it. In an industry in which products simply got cheaper every year and everything tends toward a commodity, Apple's products were able to command a premium. And in an age of pinched consumer spending, millions of people were eager — even desperate — to shell out for the latest version of the iPod, the iPad, or the iPhone.


In an era frequently characterized by executive greed and massive pay for significant underperformance, Jobs worked for a dollar a year. At a time when many founding CEOs step down when they hit their late 40s and early 50s to chase other pursuits (a la Bill Gates), Jobs stuck with it. In an era in which many experts fretted about the ability of America's economy to thrive and innovate, Apple grew into a major exporter. Apple now represents American brands, the way McDonald's and IBM and Coca-Cola once did.


In an era in which equity values stagnated, Apple's stock thrived. The performance of the company's stock, which is now worth $322 billion, up from a few billion in 2003, is one of the great examples of value creation in modern history.

It's difficult to put a tag on what it is precisely that Jobs did. He didn't create a fundamentally new business structure, the way John D. Rockefeller did with the vertical integration of Standard Oil. He didn't democratize a product that had only been available to the very rich, as Henry Ford did with the Model T. And he didn't fundamentally alter the distribution, logistics, and production systems the way that Sam Walton did with Wal-Mart. Under Jobs, Apple simply created a bunch of really cool products that people decided they needed to have. And have again. While Apple had brilliant ads, and while Jobs was an excellent salesperson, Apple's rabid, evangelizing fans have been the most effective marketing tool. When it comes to clothes, or shoes, or cars, my kids, 13 and 9, are largely indifferent to brands. When it was time for them to get their own computer, it had to be a Mac.

There are three basic business stories: the rise, the fall, and then the comeback. Jobs provided a vivid example of each. He started Apple Computer in the 1970s out of the proverbial garage with Steve Wozniak, only to be pushed after the company had gained scale. Returning to helm the company in 1997, he led a comeback that was, in many ways, far more impressive than the original rise.



Yes, Steve Jobs got rich in the past decade. But he didn't so at the expense of his shareholders. In fact, they grew rich along with him. And Apple didn't prosper at the expense of partners. The walled-garden approach of iTunes and the Apps store goes went against the grain of the notion that everything online should be free. But it was, at root, a courageous act. And it served as a kind of affirmation for content producers. And perhaps that's why he got such good press.

Several industries in the past decade found themselves essentially powerless in the face of the internet and the advent of digital technology. But Jobs and Apple invented devices and business models that encouraged people to pay: for music, for television shows and movies, for books, and for applications. By continuing to roll out new products, Apple has really expanded the playing field for content creators. It's much more compelling to watch a movie on an iPad than it is on an iPod.


The highest form of charity is helping somebody find a job or a means to support themselves. Just so, one might argue that the highest form of business is creating a profitable enterprise that allows and encourages other people to innovate and find means to support themselves. Apple has done that time and again. Yes, the publishing and music industries have griped over payment terms. But Apple is allowing individuals and companies to reach truly massive audiences at a relatively low cost. It has rescued some markets, revived others, and created entirely new ones.

This century is only a decade old. But it's a safe bet that in 2099, when analysts and historians are looking back, Steve Jobs will be remembered as one of the giants of 21st century business.


Commeents:


Steve was among the greatest of American innovators - brave enough to think differently, bold enough to believe he could change the world, and talented enough to do it.

- President Obama



He not only gave me a lot of personal advice and encouragement, he showed all of us how innovation can change lives."

- Jerry Yang, Yahoo! co-founder




For those of us lucky enough to get to work with him, it's been an insanely great honor.

- Bill Gates, Microsoft co-founder




Steve, thank you for being a mentor and a friend. Thanks for showing that what you build can change the world. I will miss you.

- Mark Zuckerberg, Facebook founder


Steve was such an 'original,' with a thoroughly creative, imaginative mind that defined an era. Despite all he accomplished, it feels like he was just getting started.

- Bob Iger, Walt Disney CEO




Monday, October 3, 2011

Msaada, msaada, msaada kwa ndugu yetu


Ramadhan Said, mkazi wa Kijiji cha Mtonga, wilayani Korogwe, anaomba wasamaria wema kumsaidia fedha za kugharimia matibabu ya miguu yake ambayo ina matatizo ya fangasi sugu.

Anasema tatizo hilo lilianza Desemba mwaka jana kwa vipele na mapunye yaliyokuwa yameota miguuni, likaendelea hadi sasa na hawezi tena kutembea au kusimama.

“Tatizo hili lilianza kama mapunye miguuni, lakini baadaye yakaanza kupanda mapajani na hatimaye tumboni,” alisema Said


Alisema alifanya juhudi za kwenda Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, ambako aliambiwa kuwa tatizo hilo ni fangasi na kupewa dawa ambazo hadi sasa hazijamsadia.

Aliongeza kwa hali inavyozidi kuwa mbaya, ni vizuri watu wakamsaidia fedha ili zimwezeshe kwenda Hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo.

“Naomba wasamaria wema wajitolee kunisaidia fedha za kunifikisha Bombo na kuniwezesha kupata matibabu kwa kuwa mimi na familia yangu hatuna uwezo huo,” alisema Said.

Alisema kwa sasa hawezi kutembea na anakabiliwa na majukumu ya familia, kwa sababu ana mke na watoto wawili ambao wanahitaji msaada wake wa hali na mali.

Kwa yeyote atakayeguswa na tatizo hili awasiliane naye kwa simu namba 0656 825139 au awasilishe mchango wake ofisi za Mwananchi zilizopo Tabata relini, Dar es salaam


Mapaka tunakomaa nao, mpaka kieleweke

Waendesha pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda, wakisubiri abiria kituo cha teksi kilichopo makutano ya Mtaa wa Likoma na Uhuru, Dar es Salaam. Bodaboda siku za karibuni zimekuwa na mivutano na wenye teksi kutokana na kutokuwa na vituo maalumu.

Libeneke la Sayansi, mpaka kieleweke

Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), kutoka kushoto ni Roselyne Sadiq, Grace Jeremia, Raudha Mwasha na Elinaike Mtei,wakiwa wameshika Laptop walizopewa na mradi wa kuhamasisha wasichana kujiunga na masomo ya sayansi na ufundi unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Italia(IDC) juzi.

Mpira wa Bongo na wachezaji wetu, kazi kwelikweli

Huyu ni mchezaji wetu wa Kitanzania, hebu angalia mwenyewe hapa ni mbele ya halaiki. Ilikuwa ni siku Taifa Stars iliporudi nyumbani baada ya kushinda nje ya nchi

Mpaka sasa bado hakijaeleweka, hatujui nani mshindi Igunga!!

Wananchi mjini Igunga wakiwa wamehudhuria mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo Jimbo la Igunga, hapa il;ikuwa ni siku ya mwisho kabla ya uchaguzi kufanyika.

Dar es Salaam bwana.. Mvua kidogo tabu tupu!

Mwendesha pikipiki akipita kwa taabu kwenye maji yaliyofurika katika eneo la Akiba jijini Dar es Salaam kufuati mvua zilizonyesha jana.

Sunday, October 2, 2011

Umri kikwazo cha Drogba Ulaya


Nyota wa Chelsea, Didier Drogba amewataka watu waache kuzungumza habari kuwa anataka kuondoka katika klabu hiyo kwa kuwa hafikirii kwenda popote.
Habari kwamba mchezaji huyo anataka kuhamia Ujerumani zilisambaa baada ya kuonekana akiwa katika tamasha la Oktoberfest Jumapili iliyopita huko Ujerumani.
Drogba alikwenda katika tamasha hilo akiwa na lengo la kuchangia katika mfuko wa watoto lakini waandishi wa habari walilipoti kwamba hiyo ilikuwa ni hatua ya kuelekea Bayern Munich mwakani.
"Habari hizo ni uzushi mtupu, katika umri kama wangu si rahisi kuanza maisha mapya katika klabu nyingine."

Waafrika wanaokimbizana kwa utajiri Ulaya


Waliondoka barani afrika kwenda Ulaya kutafuta utajiri wa pesa. Sasa wanashindana kuvuna fedha katika klabu mbalimbali kubwa barani Ulaya. Wafuatao ni wanasoka watano wa Afrika wanaoongoza kwa utajiri katika soka la Ulaya.

Samuel Etoo (Dola 40 milioni)

KABLA hajapata mkataba mnono akiwa na klabu ya Anzhi Makhchkahala ya Russia, Etoío ndiye baba wa fedha miongoni mwa wachezaji wa Afrika wakiwa huko ng'ambo.
Etoío anakadiriwa kuwa na utajiri wa Dola 40 milioni. Kwa mwaka anaingiza kiasi cha Pauni 7 milioni. Hii ilikuwa wakati akiichezea Inter Milan kabla hajasaini mkataba mpya nchini Russia ambao unamlipa mara tatu ya kiasi hicho.
Kwa mwaka jana tu, Etoío aliingiza kiasi cha Dola 15 milioni kutokana na mikataba yake ya kibiashara na Puma na Ford pamoja na mshahara wake akiwa na Inter Milan. Kwa sasa ndiye mwanasoka anayelipwa zaidi duniani akipokea kiasi cha Pauni 365,000 kwa wiki akiwa amewaacha mbali mastaa kama Cristiano Ronaldo, Lionel Messi, Carlos Tevez, Kun Aguero na wengineo.
Aliwahi kuwanunulia wachezaji, makocha na maofisa wa timu ya taifa ya Cameroon kila mmoja saa yenye thamani ya Pauni 26,000 baada ya timu hiyo kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za mwaka jana. Etoío pia huwa hachukui pesa zozote za posho anaporudi kuichezea timu ya taifa huku akijikatia mwenyewe tiketi za ndege tofauti na wachezaji wengine.

Didier Drogba (Dola 30.7 milioni)

Kwa mujibu wa gazeti la Sunday Times, Drogba ana utajiri unaokadiriwa kufikia kiasi cha Pauni 19 milioni ambazo ni sawa na Dola 30 milioni akishika nafasi ya pili nyuma ya Etoío kwa wanasoka wa Kiafrika wanaotesa Ulaya.
Kwa mshahara wa mwaka, Drogba anaingiza kiasi cha Pauni 5.5 milioni huku akiwa na mkataba unaompatia kiasi cha Pauni 105,000 kwa wiki Stamford Bridge. Drogba ana mkataba mnono na kampuni ya vinywaji baridi ya Pepsi, lakini pia ana mikataba na kampuni za Nike na Orange France.
Kudhihirisha utajiri wake, mwishoni mwa mwaka 2009, Drogba alitoa kiasi cha Pauni 3 milioni kwa ajili ya ujenzi wa hospitali katika jiji la Abidjan nchini Ivory Coast.

Michael Essien (Dola 22 milioni)


Kwa mujibu wa gazeti la Sunday Times, kiungo huyu wa kimataifa wa Ghana anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Dola 22 milioni ambazo ni sawa na Pauni 14 milioni.
Misimu miwili iliyopita, Chelsea ilimuongezea mshahara wake mpaka kufikia Pauni 80,000 kwa wiki na hilo liliongeza akaunti yake kwa kiasi kikubwa kwa mujibu wa takwimu zilizofanyika Mei mwaka huu.
Dosari kubwa katika utajiri wa Essien ni kitendo kilichoripotiwa miaka ya karibuni kuwa alikuwa amemtelekeza baba yake mzazi nchini Ghana bila ya kumjali kwa kile kinachoitwa tofauti za kifamilia. Hata hivyo kwa sasa wana maelewano mazuri na amemjengea nyumba ya kuishi.

Yaya Toure (Dola 11 milioni)

Mashine hii ya Manchester City inakadiriwa kuwa na utajiri wa Dola 11 milioni ambazo kwa pesa za Kiingereza ni sawa na Pauni 7 milioni. Yaya ni mmoja kati ya wachezaji wanaolipwa fedha nyingi duniani huku mkataba wake na Man City ukimpatia kiasi cha pauni 200,000 kwa wiki.
Mapato yake kwa mwaka yanakadiriwa kufikia Pauni 8.8 milioni lakini ataingiza Pauni 4 milioni na zaidi baada ya kukatwa kodi na serikali ya Uingereza. Hata hivyo, hapa amejumlishiwa na kiasi cha fedha alizokuwa anapata akiwa na Barcelona ya Hispania.
Baada ya kuipatia Manchester City nafasi ya kucheza katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, Toure alipata kiasi cha Pauni 800,000 kama bonasi kwa mujibu wa mkataba wake na matajiri hao wa Man City.
Pamoja na utajiri wake, Yaya hapendi maisha ya anasa na hivi karibuni aliripotiwa akiwalaumu wanasoka wengi maarufu, hasa wa Ligi Kuu England kwa kuendekeza zaidi anasa mpaka asubuhi.

Kolo Toure (Dola 11 milioni)

Kaka wa Yaya Toure ambaye kitita chake kinatoka sare na cha mdogo wake kwa sababu ghafla Yaya anavuna pesa nyingi kwa wakati mfupi wakati Kolo amevuna kwa muda mrefu tangu akiwa Arsenal.
Kolo anapokea kiasi cha Pauni 120,000 kwa wiki akiwa na Man City huku mdogo wake akipokea Pauni 200,000 kwa wiki. Kwa mwaka Kolo anaingiza kiasi cha Pauni 5.7 milioni huku akijivunia pia mkataba wake na kampuni ya Adidas.
Kolo amejikuta katika wakati mgumu baada ya kufungiwa na FA ya England kwa kufeli vipimo vya kutumia dawa za kuongeza nguvu, lakini amerudi tena uwanjani Septemba baada ya kumaliza adhabu yake ya miezi sita.