Monday, May 14, 2012

Baada ya kazi kubwa sasa ni kusherehekea kwa kwenda mbeleee!

 Wachzaji wa Manchester City wakishangilia baada ya kukabidhiwa Kombe la Ligi Kuu England
Wachzaji wa Manchester City wakipita mtaani jana Jumapili usiku baada ya mechi yao ya fainali iliyopelekea kupata ushindi wa Ligi Kuu England  baada ya kuifunga Queens Park Rangers.



Baada ya miaka 50 ya Uhuru

Wanafunzi wa darasa la sita wa Shule ya Msingi, Selous iliyopo wilayani Namtumbo, mkoani Ruvuma wakiendelea na masomo shuleni hapo. Picha na Mpigapicha Maalum       

Umewahi kuiona hii??!! Hakunaga!

Ndege aina ya Q400 NextGen kutoka Kampuni ya Bombardier ya Canada ikiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa   Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam jana, ikitafuta wateja wa kuikodisha au kuinunua. 

Tamwa yawapa somo wakuu wapya wa Wilaya


Shakila Nyerere
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(Tamwa), kimewataka Wakuu wa Wilaya walioteuliwa kuwa makini katika ufuatiliaji wa Watendaji wa Halmashauri katika shule za kata kuepukanana mimba na kufeli kwa wanafunzi wa kike nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Tamwa, Ananilea Nkya alisema wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wawe ni mifano kwa viongozi wengine walioko madarakani kufuatilia majukumu yanayozikabili jamii.
Alisema kwa takwimu walizozifanya kwa kushirikiana na wanahabari kupata takwimu hizo zilizohusu shule za kata katika mikoa 20 Bara na Visiwani kwa kila Wilaya moja katika Kata mbalimbali kwa shule 7 hadi 10 walibaini kuwa idadi kubwa ya wanafunzi wanoacha shule au kufeli ni wanafunzi wa kike.
Nkya alisema mazingira ya shule zilikojengwa ni hatari kutokana na kukosekana kwa mahitaji muhimu kwa wanafunzi kama vile Maji, miundombinu mibovu ya barabara  ni sababu mojawapo ya kuwapa vishawishi wanafunzi wa kike kuishi wakidanganyika kwa kupitia udhaifu wa maisha waliyonayo.

Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA), Ananilea Nkya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaamjana, wakati akitoa taarifa ya utafiti wa vyanzo vya ongezeko la wanafuzi kufeli mitihani ya Kitaifa.

“Wakati mwingine wanafunzi wa kike hulazimika kuishi kwa Walimu wa kiume na kuwa na mahusiano ya kimapenzi kinyume na maadili na sheria na wengine hujikuta wakiishi kwa vijana walioko mitaani kwa kutaka kujikimu kimaisha na kupata mahitaji ya kujikidhi wanapokuwa shuleni, hiyo yote ni hali za shule za kata kuwa na mapungufumengi,” alisema Nkya.
Nkya aliongeza kwa kusema mazingira ya shule za kata zilizoko mikoani na wilayani kwa upande wa walimu ni matatizo makubwa sana maana inafikiwa wakati mwingine shule yenye kidato cha kwanza hadi cha sita kuwa na walimu watatu ikiwa mwalimu wa somo la sayansi ni mmoja na kwingineko hakuna kabisa mwalimu wa somo hilo  la sayansi.
Walimu walioko wanaofundisha somo la sayansi ni mwalimu wa somo la sanaa ndiye anayefundisha sayansi kataka shule hizo.
“Ili taaluma ikue nchini hapa kinachotakiwa ni kuboresha mahitaji muhimu ikiwemo miundombinu kwa walimu na wanafunzi ikiwa ni pamoja na uwajibikaji wa viongozi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kufuatilia watendaji katika idara zao.”
Aliongeza kwa kusema wanafunzi wa kike hufeli na kukatiza masomo kwa kubeba mimba shuleni ni pamoja na kukosekana kwa walimu ambao kwa asilimia 80 wamekuwa wakishindwa kuwasili katika vituo vya kazi wanavyokuwa wamepangiwa wakikumbana na mazingira magumu kwa mara ya kwanza. 


Pale ubora unapoonekana


Mkurugenzi wa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma, akimkabidhi Laptop Zaitun Kaijage (kulia, amabaye ni mmoja kati ya washindi wa tuzo za masomo ya fani ya teknolojia ya mawasiliano katika mamlaka hiyo, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi.

Sunday, May 13, 2012

Magari ya kifahari bado yamtoa udenda Cristiano Ronaldo, ayajaza manane uani kwake


Kuwa mwanasoka ghali duniani kunafanya pesa lisiwe tatizo lako la msingi. Ni kama ilivyo kwa staa wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo. Tajiri huyu kijana ananunua chochote anachojisikia kwa sasa.

                              

Kwa mujibu wa mkataba wake, Ronaldo, analipwa kiasi cha Euro 12 milioni kwa mwaka na Real Madrid. Hii ni achilia mbali mikataba mbalimbali ya kibiashara ambayo inamwingizia mabilioni ya pesa yanayomfanya awe miongoni mwa wanasoka wanaoingiza pesa nyingi zaidi duniani kwa sasa.
Hata hivyo, ugonjwa wake wa kupenda magari ya kifahari umemfanya Ronaldo ajaze magari mengi ya bei mbaya uani kwake. Amekuwa akiyatumia mara kwenda mazoezini na katika matembezi binafsi.
Yafuatayo ni magari manane ya kifahari ambayo Ronaldo ameyajaza uani na ambayo huwa anayaendesha mara kwa mara.
                              

Bugatti Veyron
Hili ndilo gari kipenzi la Ronaldo. Bugatti Veyron ni ghali zaidi na lina mwendo wa kasi zaidi duniani. Mwendo Kasi wake wa juu huwa unafikia kilomita 407 kwa saa na linaweza kumpita dereva wa formula one anayeendesha kwa kilomita 360. Staa wa Cameroon, Samuel Eto’o ni mchezaji mwingine anayemiliki gari la aina hiyo.
Bugatti huwa linauzwa kwa oda maalumu kutoka kiwandani na mhusika analazimika kulisubiri kwa kipindi fulani wakati likitengenezwa. Linauzwa kiasi cha dola 1.2 milioni na hivyo kulifanya kuwa gari ghali zaidi duniani kwa sasa.
                              

Rolls-Royce Phantom Drophead Coupe
Rolls-Royce ni gari linaloheshimika zaidi Uingereza. Gari hili linamilikiwa na watu matajiri. Kuna watu wachache sana wanaomiliki gari hili Uingereza. Lina thamani ya dola 443,000 za Marekani.
Kinachoshangaza ni kwamba nyuma ya gari hili unaweza kufungua katika sehemu ya mizigo na kupata eneo la kukaa kufanya pikiniki.
Ukifungua kuna meza inajipandisha na kuna sehemu za kuwekea vinywaji mbalimbali.
                                

Porsche Cayenne Diesel
Gari hili limetoka Mei mwaka huu na Ronaldo alilisubiri kwa muda mrefu kulinunua moja kwa moja. Lina injini yenye nguvu na kasi yake ni kilomita 218 kwa saa. Kwa suala la mafuta, gari hili lina uwezo wa kutumia lita 10 kwa mwendo wa kilomita 100. Hili ni moja kati ya magari ya bei rahisi ambayo Ronaldo anayo. Lilimgharimu kiasi cha Euro 49,000.

                               

BMW M6
Duniani kote gari hili linatambulika kuwa ndoto ya kila mtu anayetaka kuendesha ‘Sports Car’. Kwa Ronaldo, hili ndilo gari linalomfaa zaidi kwa sababu yeye ni mwanamichezo wa hali ya juu.
Ingawa bei yake ni dola 100,000, Ronaldo hakuona shida kulinunua na kulitupia uani kwake. Ni moja kati ya magari anayotumia sana.

                                  

Porsche 911
Ni moja kati ya magari ya kifahari duniani kote. Lilimgharimu Ronaldo kiasi cha euro 201, 682 kuliweka uani kwake. Ni moja kati ya magari anayoyatumia mara kwa mara pia akienda katika starehe zake.

                                 

Bentley Continental GT
Hili ni moja kati ya magari yenye nguvu ambayo kampuni ya Bentley imewahi kuyatengeneza. Gari hili pia lina kasi kubwa huku likitumia mwendo wa kilomita 320 kwa saa. Kutokana na mapenzi yake kwa gari hili, Ronaldo alilazimika kutumia kiasi cha dola 375,000 za Marekani kwa ajili ya kulinunua na kuliweka uani kwake. Ni gari la kifahari ambalo ni ndoto ya wengi.

                                   

                                 

Ferrari F430
Gari hili la siti za watu wawili tu. Kwa sasa ndiyo dili na   Ronaldo bado ana mapenzi nalo ya dhati.
Kuna watu wanasema lishastaafishwa lakini Ronaldo hakutaka kuliuza na mpaka leo amekuwa akilitumia mara nyingi. Alitumia kitita cha dola 188,000 za Marekani kulinunua.





Audi R8
Moja kati ya magari yenye kasi duniani. Gari hili lina uwezo wa kukimbia kwa kilomita 316 kwa saa. Kwa kuliweka uwani kwake kukamilisha idadi ya magari manane ya kifahari aliyonayo, Ronaldo alilazimika kujikamua kiasi cha dola za Marekani 109,000 ili kulinunua.

Tajiri anayeishi na Papa nyumbani kwake


                                         

Bill Gates anashika nafasi ya pili katika orodha ya watu matajiri duniani. Hiyo ni kutokana na biashara yake ya kompyuta na vipuli vyake.
Anayeshika namba moja kwa utajiri duniani ni raia wa Mexico, Carlos Slim.
Gates ambaye ni Mmarekani, jina lake ni William Henry "Bill" Gates III. Alizaliwa Oktoba 28, 1955 mjini Washington, Marekani.
Ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Microsoft ambayo aliianzisha na tajiri mwenzake, Paul Allen, mwaka 1975.
Microsoft ni kampuni yenye makao yake makuu huko  Redmond, Washington, Marekani na inajishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa kompyuta na vipuli vyake duniani.
Pamoja na utajiri wake, Gates pia ni mdau mkubwa wa michezo akijihusisha na soka, gofu na tenisi.
Kupitia mfuko wake wa Bill & Belinda Foundation anashirikiana na klabu ya Barcelona ya Hispania katika kuendesha kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa polio duniani.
Kutokana na shughuli zake mbalimbali, Bill Gates ana utajiri wa Dola 61.3 bilioni (Sh5 trilioni za Kenya). Ni kati ya mabilionea wachache duniani.
Ana nyumba sehemu mbalimbali duniani lakini anaishi katika nyumba ya aina yake iliyoko katika eneo la Medina jijini Washington na liko karibu kabisa na ziwa.



                                      




Nyumba hiyo yenye vyumba vinane vya kulala,  ina thamani ya Dola 125 milioni (Sh10.2 bilioni za Kenya) na imepakana na Ziwa Washington.
James Cutler ndiye alibuni nyumba hiyo kwa kutumia mfumo wa kompyuta na aliijenga kwa kupasua mlima ulio karibu na Ziwa Washington.

                                    

Pia amejenga bwawa la samaki chini ya nyumba na limefunikwa na vioo madhubuti. Miongoni mwa samaki waliomo kwenye bwawa hilo ni pamoja na papa ambao hupita na kuonekana katika sebule ya Gates.
                                    

Gates pia ana bwawa la kuogelea kwenye nyumba yake. Bwawa hilo limefungwa vyombo vya muziki na pale mtu anapoogelea basi huburudika na muziki laini pia.
Pia mtu akiingia kwenye chumba chochote cha nyumba hiyo, taa huwaka moja kwa moja bila ya kuwashwa na mtu.
Gates ana magari kadhaa yakiwamo 1988 Porsche 959 Coupe,  1998 Lincoln Continental, 1999 Porsche 911 Convertible, Ford Focus na Limousine Chevrolet Corvette.

                                    

                                    

Pia tajiri huyo anamiliki ndege nne za kusafiria na pia ana helikopta ya kuzungukia nchini Marekani.
Miongoni mwa ndege anazomiliki Gates ni pamoja na Bombardier BD-700 Global Express ambayo bei yake ni karibu Dola 45.5 milioni.
Gates anamiliki boti yenye jina la Goygpus yenye thamani ya Dola 200 milioni .




 Tajiri huyo alimwoa Melinda French, Januari 1, 1994. Ana watoto wawili wa kike,  Jennifer Katharine Gates (1996) na Phoebe Adele (2002) na mmoja wa kiume Rory John (1999).

Nani zaidi?

Kweli kaka Kanye ameopoa mtoto wa ukweli, lakini kwangu binafsi ninapata tabu nikiangalia kati ya Kim na Amber nani mkali. Hebu angalia mwenyewe.....






Monday, April 30, 2012

Kanumba alijijua anakufa


MTAALAM wa mambo ya mwanga katika utengenezaji wa filamu Swahiliwood, Steven Shoo ëSammy Shooí, amedai kuwa marehemu Steven Kanumba alijua kuhusu kifo chake.
Hilo alilijua siku ambayo alikuwa akirekodi filamu yake ya mwisho ambayo alikuwa akirekodi filamu ya Power In Love kutokana na maneno ambayo awali walijua kama utani.
"Tukiwa tunapiga picha hizo za filamu, siku hiyo alikuwa akituhimiza tumpige picha kwa kutumia simu zetu. Nakumbuka aliniambia 'Sam nipige picha bwana, naweza kufa hapa ukakosa picha yangu ukaanza kuhangaika kuitafuta picha yangu katika Internet wakati mpo na mimi hapa... kila mtu anipige piga bwana', alisisitiza lakini katika hali ya utani," anasema Sam.
Sammy, ambaye amekuwepo na marehemu kwa muda mrefu pia na kufanya kazi na mtayarishaji mwingine Ray, anasema pamoja na kutambua kwamba Kanumba alikuwa mtu mwenye utani, lakini katika kufanya naye kazi hata siku moja hakuwahi kumsisitiza ampige picha ya ukumbusho.
Anasema, mara nyingi wanapokuwa kwenye kazi, Seth ambaye ni mdogo wake Kanumba, hupiga picha kwa ajili ya matumizi ya mtandao wake, kutokana na kusisitizwa na marehemu.


"Yaani simu yangu imejaa picha za 'location' tu nikiwa na marehemu pamoja na watendaji wengi ambao tulikuwa nao katika filamu ya mwisho aliyoigiza, siamini kama kweli bosi wetu kafariki, nahisi kama kasafiri tu kama ambavyo hufanya siku zote," anasema Sammy.

Tuesday, April 24, 2012

Hakimu ambembeleza Lulu mahakamani


Msanii wa filamu, Elizabeth Michael Kimemeta maarufu kama Lulu, jana alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu huku akibubujikwa machozi kiasi cha kumfanya Hakimu Ritha Tarimo ambembeleze ili kumnyamazisha.
Lulu anashtakiwa mahakamani hapo kwa kutuhuma za kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba na alifikishwa jana kwa mara ya pili akiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza na Polisi.
Lulu alifikishwa mahakamani hapo saa 3:06 asubuhi akiwa katika basi dogo la Magereza pamoja na mahabusu wengine wanawake ambalo lilikuwa likisindikizwa na magari mengine mawili na alikuwa chini ya ulinzi wa askari sita wa kike wa Magereza na askari mmoja wa kike wa Polisi wakishirikiana na askari wa kiume wa Magereza zaidi ya sita.
Mara baada kuingia katika chumba cha Mahakama, Lulu ambaye alikuwa amevalia dira jekundu alianza kulia kwa uchungu hali ambayo ilimlazimu Hakimu Tarimo pamoja na baadhi ya askari kumnyamazisha.
Ulinzi ulikuwa wa kufa mtu



Ilikuwa ni kazi kupata picha yake, hata JK halindwi namna hii!




Kutokana na kujaa kwa watu mahakamani hapo, askari wa Kikosi Maalumu cha Magereza walilazimika kuufunga mlango wa Mahakama hiyo ili kesi hiyo isikilizwe.
Baada ya kesi hiyo kutajwa, Wakili Mwandamizi wa Serikali Elizabeth Kaganda aliiomba Mahakama iamuru watu wote watoke nje kwa sababu walikuwa wamefunga njia ili mtuhumiwa huyo aweze kupitishwa.
Hakimu Tarimo alikubaliana na ombi hilo na kuwaamuru askari kusafisha njia ili waweze kumpitisha msanii huyo kwa kile alichosema kuwa Lulu bado ni mtuhumiwa na anaweza kuumizwa.
“Askari safisheni njia ili mtuhumiwa aweze kupita kwa sababu yeye bado ni mtuhumiwa anaweza kuumizwa,"alisema Hakimu Tarimo.
Baada ya kutolewa kwa amri hiyo, askari walitimiza wajibu wao na muda mfupi njia ilipatikana na msanii huyo kutolewa mahakamani hapo.







Jopo la mawakili
Katika kesi hiyo, Lulu anatetewa na jopo hilo la mawakili akiwemo Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), Joaquine De- Melo, Kenedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe. 
De- Melo  pia aliwahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mshindi wa Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King.
Fungamtama ambaye ndiye kiongozi wa jopo la mawakili hao wanaomtetea Lulu, anakumbukwa kwa kuitetea kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans, katika kesi dhidi ya Tanesco, ambayo alishinda na shirika hilo kuamriwa kuilipa kampuni hiyo  zaidi ya Sh94 bilioni kwa kuvunja mkataba.
Kibatala ambaye pia anamtetea kada wa Chadema, Fred Mpendazoe katika kesi ya uchaguzi Jimbo la Segerea, pia ni Makamu wa Rais wa TLS, wakati Massawe anatoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).
Mawakili hao walijitokeza jana mbele ya Hakimu Tarimo tayari kumtetea Lulu na baada ya mawakili hao kujitambulisha, Wakili Kaganda alisema upelelezi wa kesi bado haujakamilika na kuiomba Mahakama iipangie tarehe nyingine.
Hakimu Tarimo aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu itakapofikishwa mbele ya Mahakama hiyo kwa ajili ya kutajwa.
Kwa mara ya kwanza Lulu alifikishwa mahakamani hapo Aprili 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando  akikabiliwa na la shtaka hilo la mauaji. 
Wakili Kaganda alimsomea hati ya mashtaka alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu katika maeneo ya Sinza Vatican, Wilaya ya Kinondoni, mtuhumiwa alimuua  Kanumba. Kanumba alifariki dunia siku hiyo saa 9:00 usiku kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya ugomvi baina yake na Lulu.














 Hisia zikampanda
Akaanza kulia